Connect with us

News

Wito wa haki kupatikana watawala mazishi ya Albert Ojwang’

Published

on

Ibada ya mazishi kwa ajili ya mwendazake mwanablogu na mwalimu Albert Ojwang’ aliyeuawa mikononi mwa polisi inafanyika katika shule ya msingi ya Nyawango kaunti ya Homa Bay, huku kukiwa na hali ya taharuki.

Katika hafla hiyo uwepo wa maafisa wa usalama haujashuhudiwa.

Kulingana na Odhiambo Ojiro, mmoja wa wanaharakati katika eneo hilo alisema vijana wamejitolea kumpumzisha Ojwang’ kwa heshima aliyostahili’ na ishara hiyo imeonyesha umoja walionao vijana hao.

Wakizungumza katika hafla hiyo, baadhi ya walimu katika shule ambayo Albert alikuwa akihudumu katika kaunti ya Taita Taveta, wakiongozwa na Ismael Omoke Kongo walishinikiza naibu inspekta jenerali wa Eliud Lagat na wengine waliohusika na mauaji hayo kukamatwa na kufunguliwa mashtaka mahakamani.

Walisema kesi ya mauaji ya dhidi ya Albert inafaa kuchukuliwa kwa uzito na kuharakishwa mahakamani ili haki kwa familia na jamii ipatikane.

“Tunataka hii kesi kuharakishwa na wote waliohusishwa iwe kupitia kutoa maagizo hadi utekelezaji kushtakiwa”, walisema walimu hao

Wanablogu mbali mbali waliofika katika hafla hiyo waliunga mkono kauli ya walimu hao huku wakishikiniza mamlaka ya kutathmini utendakazi wa polisi IPOA na idara ya upelelezi wa makosa ya jinai DCI kuwajibika.

“Yale ambayo mnatenda Mungu anaona, ipo siku sauti zetu zitasikika, mimi naambia IPOA na DCI mnatatiza haki kwa Albert na nataka mmkamate mshtakiwa, na tunaambia serikali huwezi kutuua na utuongoze”, walisema wanablogu.

Ojwang’ alichukuliwa nyumbani kwao kaunti ya Homabay na maafisa wa usalama na kusafirishwa hadi kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi ambapo alitangazwa kufariki baadaye.

Wakati huo polisi walitoa taarifa na kudai Albert alifariki baada ya kujigonga kwenye ukuta wa chumba cha seli alimokuwa anazuiliwa kituoni Central.

Mauaji ya Albert yalizua hasira miongoni mwa wakenya hasa vijana wa kizazi cha Gen Z, ambao wamekuwa wakiendeleza misururu ya maandamano nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.

Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.

Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.

Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Published

on

By

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.

Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.

Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.

Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.

Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending