Connect with us

Business

Wito kwa Wanawake Wafanyabiashara Jijini Mombasa Kuungana na Kukuza Masoko Yao

Published

on

Wanawake wanaojishughulisha na biashara ndogondogo katika jiji la Mombasa wametakiwa kuungana kupitia vikundi ili kuimarisha masoko ya bidhaa na huduma zao, si tu ndani ya nchi bali pia kimataifa.

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Collaboration of Women in Development (CWID), Bi. Betty Sharon, amesema kuwa licha ya juhudi kubwa zinazowekwa na wanawake katika sekta ya biashara ndogondogo, bado wanakumbwa na changamoto nyingi zinazokwamisha mafanikio yao.

Bi. Sharon amesisitiza haja ya kuwajengea uwezo wanawake hao kupitia mafunzo ya kibiashara na kuwawezesha kupata raslimali muhimu kama mitaji, teknolojia, na taarifa za masoko, ili kuongeza viwango vya uzalishaji na kuvuka mipaka ya soko la ndani.

Kwa upande wao, baadhi ya wanawake wafanyabiashara wakiongozwa na Bi. Beatrice Simiyu, wameitaka serikali pamoja na wahisani kuongeza juhudi katika kuwawezesha kwa kuwapatia ujuzi wa kibiashara na miundombinu bora ya kufanikisha biashara zao.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wakaazi wahofia mkurupuko wa magonjwa baada ya kuuziwa nyama Malindi

Published

on

By

Wakaazi wa mji wa Malindi kaunti ya Kilifi wanaishi kwa hofu ya mkurupuko wa magonjwa baada ya kulalamikia kuuziwa nyama ya mifugo ambayo haijakaguliwa na maafisa wa mifugo eneo hilo.

Wakielezea manung’uniko yao, wakaazi hao walioongozwa na Kensa Ondiek walisema nyama ya mifugo inayouzwa eneo hilo haijakaguliwa, akiongeza kwamba kichinjio cha kipekee mjini humo pia kina wafanyikazi ambao ni wa umri wa chini ya miaka kumi na nane.

Wakaazi hao pia walisema mazingira ya kufanya kazi katika kichinjio hicho nai ya kutatanisha huku wachuuzi wa nyama wakifanya biashara zao mahali peupe na pachafu.

Vyombo vya Habari vilidhibitisha matukio hayo kupitia picha za watoto wakifanya kazi katika kichinjio hicho na kuchinjwa kwa mifugo siku ya Jumapili.

Afisa wa mifugo eneo la Malindi Godreck Mwaringa alitetea madai hayo akisema kwamba mifugo inayochinjwa katika kichinjio hicho hukaguliwa pindi inapofika, kabla na baada ya kuchinjwa.

Aliongezea kwamba maafisa husika hufanya kazi kuanzia siku ya Jumatatu hadi Jumamosi, japo akaweka wazi kwamba huenda wanaochinjwa siku ya Jumapili huwa ni uchinjaji wa dharura ambao pia nyama yake inafaa kukaguliwa kabla ya kuuzwa.

Hata hivyo alitoa tahadhari kwa wakazi wa Malindi kuhakikisha wananunua nyama iliyokaguliwa huku akionya kuwa watakaopatikana na mifugo wala nyama ambayo hazijakaguliwa watashtakiwa.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading

Business

Biashara ya sare za shule imedidimia Kilifi

Published

on

By

Wafanyibiashara wa kuuza sare za shule mjini Kilifi wamesema kuwa biashara hiyo iko chini msimu huu ikilinganishwa na wakati ambapo wanafunzi wakifungua shule mwezi wa kwanza.

Wakizungumza na cocofm wafanyibiashara hao walisema kuwa kwa sasa wazazi wengi hawanunui sare za shule kwa wingi ikilinganishwa na wakati ambapo shule zilikuwa zinafunguliwa kwa muhula wa kwanza.

Hata hivyo gharama ya juu ya maisha pia imetajwa kuchangia kudorora kwa biashara hiyo kwani wengi walilalamikia ukosefu wa fedha.

Walisema wanatarajia biashara hiyo kuimarika tena msimu ujao huku wakitoa wito kwa serikali kuu kuzingatia upya swala la kupanda kwa gharama ya maisha.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Trending