Connect with us

News

Waziri Ruku, aunga mkono mswada tata wa kuzuia maandamano

Published

on

Waziri wa utumishi wa umma nchini Geoffrey Ruku ameendelea kuunga mkono mswada tata wa kudhibiti mikutano na maandamano wa mwaka 2024.

Mswada huo, ambao kwa mara ya kwanza uliwasilishwa na Ruku wakati alipokuwa Mbunge wa Mbeere Kaskazini, umeibuka tena wakati huu ambapo maandamano yanayoongozwa na vijana wa kizazi cha Gen Z yanaendelea kushika kasi kote nchini.

Maandamano haya yameibua hisia kali huku vijana wakiibua masuala ya haki za binadamu, uwajibikaji wa serikali, na mustakabali wa taifa.

Waziri Ruku alitetea mswada huo, akisema kwamba mfumo wa sasa wa kisheria kuhusu mikutano na maandamano hauna nguvu za kutosha kudhibiti maandamano ya vurugu na ghasia kwani maandamano ambayo yamekuwa yakifanyika nchini yamekosa mwelekeo na uongozi thabaiti.

“Sheria ya umma ya mwaka 1952 ni ya zamani sana. Haikutungwa kwa ajili ya Kenya ya kidemokrasia na kwamba sheria mpya itanyamazisha wakenya kwa vurugu na kuwezesha maandamano ya amani, alisema Ruku.

Kulingana na Waziri huyo, mswada mpya unapendekeza kufutwa kwa sehemu ya 5 na 6 ya sheria ya agizo la umma na badala yake kuanzisha mfumo mpya wa kusimamia maandamano na mikutano ya hadhara.

Kwa mujibu wa mapendekezo ya sheria hiyo, waandamanaji watalazimika kutoa taarifa kwa polisi kati ya siku 3 hadi 14 kabla ya kufanyika kwa mkutano au maandamano yoyote.

Hata hivyo, wachanganuzi wa masuala ya kisiasa pamoja na Wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu wamekosoa vikali mswada huo, wakisema ni njama fiche ya kuzuia sauti za wananchi, hasa vijana wa kizazi cha Gen Z.

Wakosoaji hao walisema mswada huo mpya unaweza kuibua masharti magumu zaidi kwa umma kuandamana kwa amani na kwamba kuhatarisha haki ya msingi ya kujieleza na kukusanyika kwa amani.

Mswada huo unalenga kuchukua mkondo mpya baada ya Mwakilishi Kike kaunti ya Nairobi Esther Passaris kuwasilishwa mapendekezo mpya kuhusu mswada huo ambapo analenga kuzuia waandamanaji kuandamana katika maeneo yaliopigwa marufuku hasa bunge, Mahakama, ofisi kuu za umma na Ikulu pamoja na waandamanaji hao kuwa umbali wa mita 100 kutoka maeneo hayo.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama kuu yatupilia mbali ombi la Gachagua

Published

on

By

Mahakama kuu imetupilia mbali ombi la pili la aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua la kutaka jopo la majaji watatu wanaosikiliza kesi ya kupinga kubanduliwa wake mamlakani kuzuiliwa kuskiza kesi hiyo. 

Gachagua alisema kwamba majaji hao watatu akiwemo Jaji Eric Ogola, Anthony Mrima na Fridah Mugambi wanafaa kuondolewa kwenye kesi hiyo kwa misingi kwamba uteuzi wao haujazingatia sheria.

Mahakama hiyo ilitupilia mbali ombi hilo, na kusema kwamba jopo hilo la majaji watatu liliteuliwa na Jaji mkuu Martha Koome kwa kuambatana na sheria na kanuni za idara ya Mahakama.

Mahakama imeshikilia kwamba jopo hilo la majaji wa Mahakama kuu litaendelea kusikiliza kesi hiyo hadi wakati wa kutoa uamuzi kwa kuzingatia sheria, na kanuni za idara ya Mahakama pamoja na Katiba ya Kenya.

Mahakama hiyo pia ilitupilia mbali ombi la Mwanaharakati Fredrick Mula ambaye alitaka kubadilishwa kuwa mlalamishi katika kesi nne za kuondolewa mashtaka dhidi ya aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua ambazo alikuwa amewasilisha awali na kisha kutaka kujiondoa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Published

on

By

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.

Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.

Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.

“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending