Connect with us

News

Waziri Ruku, aunga mkono mswada tata wa kuzuia maandamano

Published

on

Waziri wa utumishi wa umma nchini Geoffrey Ruku ameendelea kuunga mkono mswada tata wa kudhibiti mikutano na maandamano wa mwaka 2024.

Mswada huo, ambao kwa mara ya kwanza uliwasilishwa na Ruku wakati alipokuwa Mbunge wa Mbeere Kaskazini, umeibuka tena wakati huu ambapo maandamano yanayoongozwa na vijana wa kizazi cha Gen Z yanaendelea kushika kasi kote nchini.

Maandamano haya yameibua hisia kali huku vijana wakiibua masuala ya haki za binadamu, uwajibikaji wa serikali, na mustakabali wa taifa.

Waziri Ruku alitetea mswada huo, akisema kwamba mfumo wa sasa wa kisheria kuhusu mikutano na maandamano hauna nguvu za kutosha kudhibiti maandamano ya vurugu na ghasia kwani maandamano ambayo yamekuwa yakifanyika nchini yamekosa mwelekeo na uongozi thabaiti.

“Sheria ya umma ya mwaka 1952 ni ya zamani sana. Haikutungwa kwa ajili ya Kenya ya kidemokrasia na kwamba sheria mpya itanyamazisha wakenya kwa vurugu na kuwezesha maandamano ya amani, alisema Ruku.

Kulingana na Waziri huyo, mswada mpya unapendekeza kufutwa kwa sehemu ya 5 na 6 ya sheria ya agizo la umma na badala yake kuanzisha mfumo mpya wa kusimamia maandamano na mikutano ya hadhara.

Kwa mujibu wa mapendekezo ya sheria hiyo, waandamanaji watalazimika kutoa taarifa kwa polisi kati ya siku 3 hadi 14 kabla ya kufanyika kwa mkutano au maandamano yoyote.

Hata hivyo, wachanganuzi wa masuala ya kisiasa pamoja na Wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu wamekosoa vikali mswada huo, wakisema ni njama fiche ya kuzuia sauti za wananchi, hasa vijana wa kizazi cha Gen Z.

Wakosoaji hao walisema mswada huo mpya unaweza kuibua masharti magumu zaidi kwa umma kuandamana kwa amani na kwamba kuhatarisha haki ya msingi ya kujieleza na kukusanyika kwa amani.

Mswada huo unalenga kuchukua mkondo mpya baada ya Mwakilishi Kike kaunti ya Nairobi Esther Passaris kuwasilishwa mapendekezo mpya kuhusu mswada huo ambapo analenga kuzuia waandamanaji kuandamana katika maeneo yaliopigwa marufuku hasa bunge, Mahakama, ofisi kuu za umma na Ikulu pamoja na waandamanaji hao kuwa umbali wa mita 100 kutoka maeneo hayo.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending