Connect with us

News

Wawakilishi Wadi kaunti ya Kilifi Wazibana Makonde

Published

on

Kizaazaa kilishuhudiwa katika majengo ya bunge la kaunti ya Kilifi baada ya Wawakilishi wadi ambao ni Wanachama wa Kamati ya bajeti katika bunge hilo kutofautiana kuhusu uongozi na uawajibikaji.

Hali hiyo ilisababisha Mwakilishi wadi maalum Elina Mapenzi kuzabwa makonde na Wawakilishi wadi wawili wa kiume akiwemo Mwakilishi wadi ya Shella Twahir Abdulkarim na Mwakilishi wadi ya Watamu Ibrahim Matumbo ambao wanaegemea upande wa Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro wakati wa kikao cha kutathmini masuala tata kuhusu bajeti ya mwaka wa kifedha 2025/26.

Kulingana na baadhi ya Wawakilishi wadi waliokuwa katika kikao hicho, kizaazaa hicho kilisababisha Mwakilishi wadi huyo maalum kupata majeraha wakati wa vurugu hizo kwenye kikao hicho cha kamati ya bajeti.

Kizaazaa hicho pia kilichangiwa zaidi pale wanachama wa kamati hiyo walipochukizwa na hatua ya Spika wa bunge hilo Teddy Mwambire kuagiza bunge kujadili mchakato wa bajeti ya mwaka huu bungeni na wala sio kamati hiyo ya bajeti kwa kuambatana na sheria.

Wawakilishi wadi hao, sasa wanadai kwamba watawasilisha hoja bungeni ya kutokuwa na Imani na Spika Mwambire ili kumtimua uongozini kwa kukiuka kanuni za bunge hilo.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Shirika la Kilifi Mum’s Kibibi Ali amekashfu vikali kitengo hicho, akikitaja kama unyanyasaji wa kijinsia kwa viongozi wa kike katika kaunti hiyo.

Continue Reading
Click to comment

0 Comments

  1. Nasser Mohammed

    May 14, 2025 at 11:33 am

    Kuna barua nimemuandikia spika kama mwananchi mzalendo,naomba ni share na nyinyi tafadhali.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mwanaharakati Mwabili Mwagodi apatikana

Published

on

By

Mwanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu Mwabili Mwagodi ambaye alidaiwa kutekwa nyara akiwa nchini Tanzania sasa amepatikana.

Mkurugenzi wa Shirika la kutetea haki za kibinamu nchini la VOCAL Africa Hussein Khalid, alisema Mwabili alipatikana katika msitu wa Kinondo eneo bunge la Msambweni kaunti ya Kwale mwendo wa saa tisa usiku akitembea kuelekea Diani.

Khalid alisema Mwabili, anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Pandya mjini Mombasa kisha baadaye atasafirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi kuungana na familia yake.

“Tunashukuru Mwabili amepatikana akiwa hai japo amedhohofika na anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Pandya na kisha atarudi Nairobi kukutana na familia yake lakini tunaiambia serikali ya Kenya na Tanzania ni lazima wahusika kukomesha tabia hii ya kuwateka watu nyara kuna sheria kama mtu amekosea apelekwe Mahakamani”, alisema Khalid.

Hata hivyo Wanaharakati hao wa kutetea haki za kibinadamu waliishtumu serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuwanyanyasa wanaharakati wa kijamii wa taifa la Tanzania na wale wanaoingia Tanzania kutoka mataifa mengine ili kuendeleza hamasa za haki za kijamii.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Kesi ya mauaji ya mfanyabiashara Herman yahairishwa

Published

on

By

Kesi ya mauaji ya mfanyabiashara ambaye ni raia wa Uholanzi, Rowenhorst Herman na mlinzi wake Evans Bokoro imeahirishwa hadi mwezi Oktoba mwaka huu kufuatia Mahakama kuingia kwenye mapumziko rasmi ya majaji.

Mke wa Marehemu, Riziki Cherono pamoja na mshukiwa mwenza Timothy Omondi wanakabiliwa na mashtaka ya kupanga na kutekeleza mauaji hayo yaliyotokea Juni 4 mwaka 2021 katika eneo la Shanzu kaunti ya Mombasa.

Katika kikao cha awali cha Mahakama, Afisa wa Polisi Koplo Richard Cheruiyot alieleza mbele ya Jaji Wendy Micheni kwamba Cherono alijaribu kuonekana kama mwathirika kwa madai ya kutekwa nyara na majambazi waliodaiwa kuvamia nyumba yao.

Afisa huyo alieleza kwamba walimkuta Cherono akiwa amefungwa kwenye usukani wa gari lake, huku akidai kwamba alivamiwa na kulazimishwa kuondoka nyumbani kwao akiwa chini ya tishio la bunduki.

Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa ulibaini kwamba Marehemu Herman alipatikana amefariki nyumbani kwake akiwa amefungwa mikono na miguu huku mlinzi wao, Evans Bokoro, alikutwa akiwa hai kwa taabu karibu na bwawa la kuogelea lakini baadaye alifariki akipelekwa hospitalini.

Mashahidi wa upande wa mashtaka pamoja na polisi, wanaamini kwamba Cherono ndiye mshukiwa mkuu wakidai kwamba alipanga na kufanikisha mauaji hayo kwa kushirikiana na watu wengine, wakiwemo waliotajwa kuwa sehemu ya genge lililovamia nyumba hiyo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending