Connect with us

News

Wawakilishi Wadi kaunti ya Kilifi Wazibana Makonde

Published

on

Kizaazaa kilishuhudiwa katika majengo ya bunge la kaunti ya Kilifi baada ya Wawakilishi wadi ambao ni Wanachama wa Kamati ya bajeti katika bunge hilo kutofautiana kuhusu uongozi na uawajibikaji.

Hali hiyo ilisababisha Mwakilishi wadi maalum Elina Mapenzi kuzabwa makonde na Wawakilishi wadi wawili wa kiume akiwemo Mwakilishi wadi ya Shella Twahir Abdulkarim na Mwakilishi wadi ya Watamu Ibrahim Matumbo ambao wanaegemea upande wa Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro wakati wa kikao cha kutathmini masuala tata kuhusu bajeti ya mwaka wa kifedha 2025/26.

Kulingana na baadhi ya Wawakilishi wadi waliokuwa katika kikao hicho, kizaazaa hicho kilisababisha Mwakilishi wadi huyo maalum kupata majeraha wakati wa vurugu hizo kwenye kikao hicho cha kamati ya bajeti.

Kizaazaa hicho pia kilichangiwa zaidi pale wanachama wa kamati hiyo walipochukizwa na hatua ya Spika wa bunge hilo Teddy Mwambire kuagiza bunge kujadili mchakato wa bajeti ya mwaka huu bungeni na wala sio kamati hiyo ya bajeti kwa kuambatana na sheria.

Wawakilishi wadi hao, sasa wanadai kwamba watawasilisha hoja bungeni ya kutokuwa na Imani na Spika Mwambire ili kumtimua uongozini kwa kukiuka kanuni za bunge hilo.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Shirika la Kilifi Mum’s Kibibi Ali amekashfu vikali kitengo hicho, akikitaja kama unyanyasaji wa kijinsia kwa viongozi wa kike katika kaunti hiyo.

Continue Reading
Click to comment

0 Comments

  1. Nasser Mohammed

    May 14, 2025 at 11:33 am

    Kuna barua nimemuandikia spika kama mwananchi mzalendo,naomba ni share na nyinyi tafadhali.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.

Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.

Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.

Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Published

on

By

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.

Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.

Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.

Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.

Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending