Connect with us

News

Wavuvi wataka KPA kumwaga tope eneo mbadala baharini

Published

on

Wavuvi eneo bunge la Likoni, kaunti ya Mombasa, wameitaka halmashauri ya bandari nchini (KPA) kusitisha mara moja shughuli za kumwaga tope maeneo ya bahari wanakofanyia shughuli zao za uvuvi.

Wavuvi hao walisema tope hizo zimeathiri mazingira ya bahari na kuhatarisha maisha ya viumbe hai majini, hasa samaki ambao ni tegemeo lao kuu la kipato.

Wakizungumza wakati wa kikao cha hadhara cha kukusanya maoni ya wananchi kuhusu uandaaji wa mpango wa maendeleo ya kaunti wa mwaka wa fedha 2026/2027 wavuvi hao walieleza kuwa tope hizo zinatokana na upanuzi wa kina cha bandari, na kumwaga tope baharini kunasababisha uchafuzi wa maji na kuharibu mazalia ya samaki.

Wakiongozwa na Shaban Mohammed, waliitaka KPA kushirikiana na jamii za wavuvi kabla ya kutekeleza miradi yoyote inayohusisha maeneo ya bahari, na kutumia mbinu mbadala za utupaji wa tope zinazolinda mazingira na maisha ya wakazi.

“Wale watu wanaokuja kuchimba kula bandarini wanamwaga tope kwenye mazingira ya samakai ambako ndio maeneo tunavua samaki, hatujui ni eneo walipewa na wanaochimba kule au ni wao wenyewe wanafanya hivyo kwa sababu hawafiki mahali stahiki ya kumwaga zile taka”,alisema Mohammed

Aidha, gavana wa Mombasa, Abdulswamad Sharif Nassir, aliahidi kufuatilia suala hilo na taasisi husika ili kuhakikisha linaangaziwa na kutatuliwa kwa haraka.

Taarifa ya Mwanahabari.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu wakamatwa, Malindi

Published

on

By

Maafisa wa polisi Malindi kaunti ya Kilifi wanasema wamewanasa washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu katika msako kwenye mitaa ya Karima, Soweto, Milano na Mgandini.

Polisi ilisema msako huo umewawezesha kuwakamata washukiwa 11 wa genge la “Wakali Mwisho” na wanawake watano kwa visa vya utovu wa nidhamu.

Msako huo unafuatia zaira ya kamanda wa polisi ukanda wa pwani Ali Nuno katika eneo hilo na kuwataka polisi kuongeza juhudi za kukabiliana na wanachama wa magenge hayo wanaoendelea kuwahangaisha wananchi.

Simu 14 zilizoshukiwa kuwa za wizi zilinaswa kutoka kwa mshukiwa Ahmed Ali.

Magenge ya uhalifu wakiwemo wale wanaojiita mawoza ni miongoni mwa makundi ya vijana ambao wamekuwa wakitatiza amani na usalama miongoni mwa wakaazi eneo hilo.

Idara ya usalama ilikuwa mbioni kuwasaka wahalifu katika mji huo wa kitalii katika juhudi za kurejesha amani na utulivu.

Vijana hao wamekuwa wakiwavamia wakaazi na kutekeleza vitendo vya wizi.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Mabadiliko ya tabianchi yatajwa kuchangia mapato duni ya samaki, Lamu

Published

on

By

Wadau katika sekta ya mazingira kaunti ya Lamu wanasema mabadiliko ya hali ya anga yanayoshuhudiwa sawa na ujenzi wa bandari ya Lamu kumechangia mapato ya samaki kupungua katika bahari hindi.

Mahmoud Yusuf ambaye ni mwanazingira alisema zana za kizamani wanazotumia wavuvi kuvua samaki pia zinachangia mapato duni ya samaki.

Yusuf alisema tangu ujenzi huo wa bandari uanze, maji ya bahari chini yamekuwa na matope kutokana na kuchimbwa na kufukuliwa kwa bahari, hali iliyochangia samaki kutorokea bahari kuu.

Mwanamazingira huyo aliitaka serikali kuwapa wavuvi vifaa vya kisasa vya uvuvi sawa na meli za uvuvi zitakazowawezesha kufika maji makuu, baada ya bandari ya ndani kuharibika.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

Trending