News
Watu 4 waaga dunia wakati wa Sabasaba

Watu wanne wamethibitishwa kuaga dunia wakati wa maandamano ya kuadhimisha miaka 35 ya kumbukumbu za Sabasaba ambapo watu 2 wamepiga risasi na kufariki katika maeneo ya Kitengela, wawili katika maeneo ya Kangemi na mtu mmoja katika maeneo ya Olkalou.
Kamanda wa Polisi kaunti ya Nyandarua Stellah Cherono alithibitisha kupigwa risasi kwa mkaazi wa Olkalou kaunti ya Nyandarua, akisema mtu huyo alipigwa risasi na kufariki wakati wa makabiliano kati ya maafisa wa polisi na waandamanaji.
Cherono aliwaonya vijana dhidi ya kuwashambulia maafisa wa polisi, akisema jukumu la maafisa wa polisi ni kuhakikisha usalama unaimarishwa lakini vijana wamekosa busara na kushambulia maafisa wa polisi kwa mawe.
Tayari mashirika ya kutetea haki za kibinadamu yameikosoa serikali kwa kuendelea kushuhudiwa kwa maafa ya kila wakati wa maandamano, wakisema serikali ni lazima iheshimu katiba ya nchi ambayo inaruhusu maandamano ya amani.
Hata hivyo baada ya wakenya waliyojeruhiwa vibaya wanaendelea kupokea matibabu katika hospitali mbalimbali huku Shirika la Msalaba Mwekundi nchini likisema idadi ya wale waliojeruhiwa inazidi kuongezeka.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.
Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.
Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.
Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.
“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.
Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.
Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.
“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.
Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.
Taarifa ya Janet Mumbi