Connect with us

News

Watoto wa umri wa miaka 14 na 16 watoa ushahidi dhidi ya Mackenzie

Published

on

Mashahidi wawili wa umri mdogo wameelezea Mahakama ya Mombasa ukatili waliopitia mikononi mwa wazazi wao kufuata maagizo ya mchungaji Paul Mackenzie katika kesi ya mauaji inayomkabili pamoja na washukiwa wengine 94.

Mtoto wa kwanza mwenye umri wa miaka 16 alisimulia jinsi mamake alivyomuondoa shuleni baada ya kufuata mafundisho ya Mackenzie kupitia runinga, kuuza mali ya nyumbani ili kufadhili safari yao hadi msitu wa Shakahola.

Aidha alieleza Mahakama kwamba wakiwa njiani walifungiwa kwenye hema na kulazimishwa kufunga kwa imani ya kuharakisha safari ya kwenda mbinguni na pia jinsi alivyoadhibiwa vikali kwa kuiba chakula kutokana na njaa na hatimaye kutoroka kwa msaada wa wazee wa kijiji.

Shahidi wa pili, ambaye ni mtoto wa miaka 14, alielezea Mahakama jinsi walivyonyimwa haki ya kwenda shule kwa madai kuwa elimu ni ya kishetani, akieleza kwamba waliwekewa vizuizi vya kutoka nje huku Chifu wa eneo hilo akifanya ukaguzi wa wanafunzi.

Mashahidi hao pi walielezea ibada, mikutano ya maombi na kufunga kwa lazima chini ya uongozi wa Mackenzie, ambapo mazishi yalijulikana kama “harusi.”

Kesi hiyo itaendelea lhuku mashahidi zaidi wakitarajiwa kufika Mahakamani mbele ya Hakimu mkuu Alex Ithuku.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama kuu yatupilia mbali ombi la Gachagua

Published

on

By

Mahakama kuu imetupilia mbali ombi la pili la aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua la kutaka jopo la majaji watatu wanaosikiliza kesi ya kupinga kubanduliwa wake mamlakani kuzuiliwa kuskiza kesi hiyo. 

Gachagua alisema kwamba majaji hao watatu akiwemo Jaji Eric Ogola, Anthony Mrima na Fridah Mugambi wanafaa kuondolewa kwenye kesi hiyo kwa misingi kwamba uteuzi wao haujazingatia sheria.

Mahakama hiyo ilitupilia mbali ombi hilo, na kusema kwamba jopo hilo la majaji watatu liliteuliwa na Jaji mkuu Martha Koome kwa kuambatana na sheria na kanuni za idara ya Mahakama.

Mahakama imeshikilia kwamba jopo hilo la majaji wa Mahakama kuu litaendelea kusikiliza kesi hiyo hadi wakati wa kutoa uamuzi kwa kuzingatia sheria, na kanuni za idara ya Mahakama pamoja na Katiba ya Kenya.

Mahakama hiyo pia ilitupilia mbali ombi la Mwanaharakati Fredrick Mula ambaye alitaka kubadilishwa kuwa mlalamishi katika kesi nne za kuondolewa mashtaka dhidi ya aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua ambazo alikuwa amewasilisha awali na kisha kutaka kujiondoa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Published

on

By

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.

Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.

Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.

“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending