News
Watoto wa umri wa miaka 14 na 16 watoa ushahidi dhidi ya Mackenzie

Mashahidi wawili wa umri mdogo wameelezea Mahakama ya Mombasa ukatili waliopitia mikononi mwa wazazi wao kufuata maagizo ya mchungaji Paul Mackenzie katika kesi ya mauaji inayomkabili pamoja na washukiwa wengine 94.
Mtoto wa kwanza mwenye umri wa miaka 16 alisimulia jinsi mamake alivyomuondoa shuleni baada ya kufuata mafundisho ya Mackenzie kupitia runinga, kuuza mali ya nyumbani ili kufadhili safari yao hadi msitu wa Shakahola.
Aidha alieleza Mahakama kwamba wakiwa njiani walifungiwa kwenye hema na kulazimishwa kufunga kwa imani ya kuharakisha safari ya kwenda mbinguni na pia jinsi alivyoadhibiwa vikali kwa kuiba chakula kutokana na njaa na hatimaye kutoroka kwa msaada wa wazee wa kijiji.
Shahidi wa pili, ambaye ni mtoto wa miaka 14, alielezea Mahakama jinsi walivyonyimwa haki ya kwenda shule kwa madai kuwa elimu ni ya kishetani, akieleza kwamba waliwekewa vizuizi vya kutoka nje huku Chifu wa eneo hilo akifanya ukaguzi wa wanafunzi.
Mashahidi hao pi walielezea ibada, mikutano ya maombi na kufunga kwa lazima chini ya uongozi wa Mackenzie, ambapo mazishi yalijulikana kama “harusi.”
Kesi hiyo itaendelea lhuku mashahidi zaidi wakitarajiwa kufika Mahakamani mbele ya Hakimu mkuu Alex Ithuku.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Mudavadi: Mazungumzo yanaendelea kuhusu mzozo wa Kenya na Tanzania

Mzozo kati ya Kenya na Tanzania umeanza kutokota kufuatia ilani iliyotolewa siku ya Jumanne Julia 29, na serikili ya Muungano wa Jumhuri ya Tanzania.
Serikali hiyo ya Tanzania kupitia Waziri wa Biashara na viwanda nchini humo Selemani Jefo ilitoa ilani ya kuwazuia wafanyibiashara wa kigeni kuendelea kufanya baadhi ya biashara katika taifa hilo.
Kutokana na hilo, Waziri wa masuala ya kigeni nchini Musalia Mudavadi alisema juhudi zimeanza za kuishawishi serikali ya Tanzania kuondoa vikwanzo hivyo na kwamba Rais William Ruto anafanya mazungumzo na mwenzake wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuhusu suala hilo.
“Rais William Ruto ambaye ni Mwenyekiti wa Jumaiya ya Afrika Mashariki anafanya mazungumzo na rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan na mwafaka utapatikana kwani pia suala la diplomasia ni mwafaka na hii tatizo tutatua kama serikali kupitia mazungumzo ya kidiplomasia”, alisema Mudavadi.
Kwa upande wake Waziri wa biashara na viwanda nchini Lei Kinyanjua alionya kwamba huenda serikali ya Kenya ikachukua hatua sawa na hiyo dhidi ya Tanzania iwapo taifa hilo la Afrika Mashariki halitaangazia upya vikwanzo hivyo.
Mzozo huo wa kidiplomasia umejiri siku moja tu baada ya Waziri wa biashara na viwanda nchini Tanzania Selemani Jafo kutangaza kwamba serikali ya Tanzania imepiga marufuku wafanyibiashara wa kigeni dhidi ya kufanya biashara ndogo ndogo nchini humu ili kuruhusu watanzania kujiimarisha kiuchumi.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Ethekon: Sheria haijafafanua taratibu za kuwarudisha nyumbani wabunge

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imeweka wazi kwamba hakuna sheria inayofafanua misingi na taratibu za kuwarudisha nyumbani wabunge ama maseneta waliokosa kuwajibikia majukumu yao ya kikazi.
IEBC, ilieleza kwamba suala hilo ni kinyume cha Katiba na ubaguzi ikilinganisha hatua hiyo na uamuzi uliyotolewa na Mahakama kuu kuhusu kesi iliyowasilishwa Mahakamani na Taasisi ya Katiba dhidi ya Ofisi ya Mwanasheria mkuu kwa kuambatana na sheria ya uchaguzi ya 2011.
Katika taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na kutiwa saini na Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon, IEBC ilisema kutokana na kwamba hakuna mfumo wa sheria wa kuwarudisha nyumbani wabunge ama maseneta waliokosa kuwajibikia majukumu yao ya kikazi, wakenya wanaweza kutumia kipengele cha 104 cha Katiba na kuwarudisha nyumbani Wawakilishi wadi.
Aidha alisema wakati bunge la kitaifa likifanya marekebisho ya sheria kuruhusu kurudishwa nyumbani Wawakilishi wadi, hakuna mwafaka wowote uliafikiwa wa kuruhusu wabunge kurudishwa nyumbani iwapo wamekosa kuwajibika.
Hata hivyo Tume hiyo imeahidi kuwajibika kikamilifu katika suala hilo huku ikisema tayari imeliandikia barua bunge la kitaifa kuibuka na sheria ya kuwarudisha nyumbani wabunge wasiowajibika.
Haya yamejiri kufuatia malalamishi yaliowasilishwa na baadhi ya wakenya wanaotaka baadhi ya wabunge na maseneta kurudishwa nyumbani wa hivi karibuni akiwa Mwakilishi wa Kike kaunti ya Nairobi Esther Passaris akituhumiwa kuvunja sheria na kukiukaji wa Katiba lakini uamuzi wa Tume ya IEBC ni afuani kwake.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi