Connect with us

News

Watene: CBC itawafaidi wakenya iwapo itaangazia changamoto za wananchi.

Published

on

Mgombea wadhifa wa urais katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2027 Robert Watene amesema mfumo wa mtaala wa elimu nchini CBC utawafaidi wakenya iwapo utaangazia changamoto wanazokumbana nazo wakenya.

Akizungumza katika mahojiano ya kipekee na Coco FM, Watene amesema nchi ya Kenya imesalia nyuma kielimu na kimaendeleo tofauti na nchi zingine kwani mfumo uliyopo nchini haujampa mtoto ujuzi wa kumasaidia kujiajiri baada ya masomo.

Akitolea mfano nchi ya Ujerumani, Watene amesema mfumo wao huangazia kuwapa wanafunzi ujuzi jambo ambalo kulingana naye limepunguza ongezeko la ukosefu wa ajira nchini humo.

“Masomo ya nje wanafocus sana na problem za kwao hata ukiangalia zile curriculum zao zinajaribu kusolve zile matatizo ambazo wako nazo unapata mtu amemaliza kusoma na tayari ako na skill ya kutengeneza magari na kadhalika” alisema Robert Watene.

Watene amesema mfumo mpya wa CBC unastahili kuwa kama vyuo vya kiufundi ili kuwasaidia vijana kujiajiri pindi tu wanapokamilisha masomo yao.

Wakati uo huo amesema iwapo atapata nafasi ya kuongoza taifa la Kenya atahakikisha anabadilisha maji ya bahari kuwa maji safi kwa matumizi ya binadamu ili kuwapunguzia dhiki wakaazi wa eneo la Pwani.

“There people who are walking kilometers and kilometers to get water ila hakuna kiongozi ambaye amesimama kuhakikisha kwamba haya maji yetu ya bahari yanageuka maji safi ya kunywa ili kupunguza magonjwa yanayosababishwa na maji chafu” alidokeza Watene.

Taarifa ya Elizabeth Mwende.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mwanaharakati Mwabili Mwagodi apatikana

Published

on

By

Mwanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu Mwabili Mwagodi ambaye alidaiwa kutekwa nyara akiwa nchini Tanzania sasa amepatikana.

Mkurugenzi wa Shirika la kutetea haki za kibinamu nchini la VOCAL Africa Hussein Khalid, alisema Mwabili alipatikana katika msitu wa Kinondo eneo bunge la Msambweni kaunti ya Kwale mwendo wa saa tisa usiku akitembea kuelekea Diani.

Khalid alisema Mwabili, anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Pandya mjini Mombasa kisha baadaye atasafirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi kuungana na familia yake.

“Tunashukuru Mwabili amepatikana akiwa hai japo amedhohofika na anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Pandya na kisha atarudi Nairobi kukutana na familia yake lakini tunaiambia serikali ya Kenya na Tanzania ni lazima wahusika kukomesha tabia hii ya kuwateka watu nyara kuna sheria kama mtu amekosea apelekwe Mahakamani”, alisema Khalid.

Hata hivyo Wanaharakati hao wa kutetea haki za kibinadamu waliishtumu serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuwanyanyasa wanaharakati wa kijamii wa taifa la Tanzania na wale wanaoingia Tanzania kutoka mataifa mengine ili kuendeleza hamasa za haki za kijamii.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Kesi ya mauaji ya mfanyabiashara Herman yahairishwa

Published

on

By

Kesi ya mauaji ya mfanyabiashara ambaye ni raia wa Uholanzi, Rowenhorst Herman na mlinzi wake Evans Bokoro imeahirishwa hadi mwezi Oktoba mwaka huu kufuatia Mahakama kuingia kwenye mapumziko rasmi ya majaji.

Mke wa Marehemu, Riziki Cherono pamoja na mshukiwa mwenza Timothy Omondi wanakabiliwa na mashtaka ya kupanga na kutekeleza mauaji hayo yaliyotokea Juni 4 mwaka 2021 katika eneo la Shanzu kaunti ya Mombasa.

Katika kikao cha awali cha Mahakama, Afisa wa Polisi Koplo Richard Cheruiyot alieleza mbele ya Jaji Wendy Micheni kwamba Cherono alijaribu kuonekana kama mwathirika kwa madai ya kutekwa nyara na majambazi waliodaiwa kuvamia nyumba yao.

Afisa huyo alieleza kwamba walimkuta Cherono akiwa amefungwa kwenye usukani wa gari lake, huku akidai kwamba alivamiwa na kulazimishwa kuondoka nyumbani kwao akiwa chini ya tishio la bunduki.

Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa ulibaini kwamba Marehemu Herman alipatikana amefariki nyumbani kwake akiwa amefungwa mikono na miguu huku mlinzi wao, Evans Bokoro, alikutwa akiwa hai kwa taabu karibu na bwawa la kuogelea lakini baadaye alifariki akipelekwa hospitalini.

Mashahidi wa upande wa mashtaka pamoja na polisi, wanaamini kwamba Cherono ndiye mshukiwa mkuu wakidai kwamba alipanga na kufanikisha mauaji hayo kwa kushirikiana na watu wengine, wakiwemo waliotajwa kuwa sehemu ya genge lililovamia nyumba hiyo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending