Connect with us

News

Mahakama ya Shanzu kubaini hatma ya Washukiwa wa wizi, Mtwapa

Published

on

Washukiwa 7 waliokamatwa katika eneo la Mtwapa kaunti Kilifi kwa tuhuma za wizi kwenye magari watafahamu hatma yao siku ya Ijumaa 13 mwezi huu iwapo wataachiliwa kwa dhaman au la.

Washukiwa hao Edwin Kyalo Mulandi, Nicholus Mungaro Kitumbo maarufu Papa, Erick Kabue Maranga maarufu Wachira, Ali Said Nassir, Fred Mungoma Mwanjira, Fredrick Kalungo Konde na Akasha Hassan Akasha walifikishwa katika Mahakama ya Shanzu kaunti ya Mombasa ambako walikanusha mashtaka dhidi yao.

Aidha, upande wa mashtaka uliwasilisha ombi la kutaka saba hao kunyimwa dhamana ikizingatiwa kwamba ni miongoni mwa wahalifu sugu ambao walikuwa wakitafutwa na asasi za usalama, baadhi yao wakiwa na rekodi za kesi Mahakamani.

Saba hao walikamatwa baada ya kuhusishwa na visa vya wizi viliyoripotiwa katika vituo mbalimbali vya polisi ikiwemo Mtwapa kaunti ya Kilifi, Changamwe, Nyali, Tononoka, Makupa na Central, kaunti ya Mombasa, kituo cha Embakasi jijini Nairobi na Dar es Salaam nchini Tanzania.

Wakati wa kukamatwa 7 hao, polisi pia walifanikiwa kunasa magari 8 na bidhaa mbalimbali zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 7.

Taarifa ya Mwanahabari wetu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Published

on

By

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.

Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.

“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi

Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.

Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending