Connect with us

Sports

Wanandondi Mombasa Kuingia Kambini

Published

on

Chama cha Ndondi kaunti ya Mombasa (MCBA) kinatarajia kuanza rasmi kambi ya mafunzo, hii leo  katika taasisi ya Alliance Française huko Nyali, kama sehemu ya maandalizi kuelekea ligi ya kitaifa ya ndondi inayotarajiwa kuanza tarehe 17 hadi 19 Julai mwaka huu.

Kambi hiyo  italeta pamoja wakufunzi 10 kutoka jijini Mombasa wakishirikiana na wataalam wawili wa kimataifa ambao ni Franck Petitjean bingwa wa zamani wa Ulaya na bingwa wa mara nne wa Ufaransa pamoja na Valentino Gargiulo mtaalamu wa hali ya mwili kwa wanamichezo

Kambi hii inazinduliwa juu ya mafanikio ya mradi wa ndondi mashinani, mradi wa pamoja kati ya Kenya na Ufaransa uliozinduliwa mwezi Mei mwaka huu, ukiwa na lengo la kuwapa vijana mafunzo, kuwawezesha makocha, na kuandaa mabondia mahiri kwa ushindani wa kimataifa.

Kwa sasa, Mombasa inaweka mikakati ya kuibuka na ushindi katika Ligi ya Kitaifa, kambi hii ikiwa ni sehemu ya safari hiyo ya mafanikio.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Published

on

By

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Continue Reading

Sports

Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading

Trending