Connect with us

Business

Wakulima wa Mahindi Chonyi Wakadiria Hasara Kutokana na Mvua Kubwa

Published

on

Baadhi ya wakulima wa mahindi katika eneo la chonyi kaunti ya kilifi wanakadiria hasara kutokana na mvua nyingi ambayo inaendelea kunyesha maeneo mengi nchini.

Kulingana na wakulima hao hasa ambao mashamba yao yako karibu na mito mahindi waliyopanda hayastahimili mvua nyingi hivyo kuwasababishia hasara kutokana na kuharibika .

Wanasema mahindi mengine yamesombwa na maji hali ambayo imeawasabashia hasara na kuitaka serikali kuwasambazia mbegu ambazo zinaweza kustahimili mvua nyingi ili waweze kuendeleza kilimo biashara bila changamoto zozote ikizingatiwa wanategemea kilimo kujikimu kimaisha.
“ mashamba yamejaa maji kila mahali hali ambayo imefanya mahindi kuoza na hata kuchomeka hasa sisi ambao mashamba yetu yako karibu na mito hatutapata chocote kabisa”

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Kenya kuzindua utalii wa anga (Astro-tourisim)

Published

on

By

Kenya itakuwa mwenyeji wa uzinduzi wa utalii wa anga(Astro-tourisim) katika kaunti ya Samburi Septemba 7, 2025, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha na kubadilisha aina za utalii nchini.

Uzinduzi huo unaendana sambamba na tukio la mwezi kupatwa maarufu kama Blood moon ambapo litaanza saa mbili na nusu usiku wa septemba 7, 2025, na kudumu kwa dakika 82.

Mpango huu wa kipekee unalenga kuifanya Kenya kuwa kivutio kikuu cha wapenzi wa sayansi ya anga na wasafiri wa kimataifa wanaopenda maajabu ya siri.

Kwa mujibu wa  shirika la Magical Kenya, tajriba hii ya anga inalenga kutumia mazingira ya kipekee ya nchi kufungua ukurasa mpya na endelevu wa utalii.

Waziri wa utalii na wanyama pori Rebecca Miano atakuwa mgeni rasmi akiandamana na wageni wa kimataifa katika hafla hiyo itakayofanyika katika Sopa Lodge kwenye hifadhi ya kitaifa ya Samburu.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Business

Mradi wa kiuchumi wa Dongo Kundu wavutia wawekezaji zaidi

Published

on

By

Wawekezaji wa ndani na nje ya nchi wanaendelea kuonyesha nia ya kuekeza katika mradi wa kiuchumi wa dongo kundu kaunti ya Mombasa.

Mradi huo unaotarajiwa kuongeza uzalishaji katika viwanda na thamani ya bidhaa ndani ya nchi na nje, unatarajiwa kukamilika hivi karibuni.

Kampuni ya nishati kutoka China, Ruike Energy Group Limited, ni mwekezaji wa hivi karibuni kuonyesha nia ya kupata nafasi ndani ya eneo hilo la kiuchumi la Dongo Kundu kwa ajili ya kuanzisha kiwanda cha kusafisha mafuta.

Kulingana na halmashauri ya bandari nchini KPA hatua hiyo italeta faida Zaidi ikiwemo kubuni nafasi za ajira, ikuaji wa uchumi, upatikanaji wa vifaa vya baharini, na urahisi wa kufikia masoko ya kanda na ya kimataifa.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Trending