Connect with us

News

Wakulima Kilifi wanufaika na Ng’ombe wa maziwa.

Published

on

Serikali ya kaunti ya Kilifi kupitia idara ya kilimo imeanzisha mpango wa kusambaza wa Ng’ombe wa maziwa kwa makundi ya wakulima wa mifugo kaunti hiyo.

Akizungumza na wanahabari wakati wa zoezi la ugavi wa ng’ombe hao eneo la Kakuyuni, waziri wa kilimo kaunti ya Kilifi Chula Mwagona alibainisha kuwa tayari jumla ya Ng’ombe 150 wamesambazwa katika maeneo mbalimbali ya kaunti hiyo kwa wafugaji.

Mwagona alikariri kuwa mradi huo unalenga kusambaza takriban ng’ombe 500 kwa makundi ya wafugaji ifikapo mwishoni mwa mpango huo.

“Kaunti ya kilifi idadi ya ng’ombe ambao tumesambaza inafika zaidi ya 150, kila kundi linapata ng’ombe 30 na saa hii tuko na makundi 17”, alisema Mwagona.

Wakati huo huo waziri huyo alidokeza kuwa mradi huo utapunguza pakubwa tatizo la uhaba wa maziwa ambao umekuwa ukikumba kaunti ya Kilifi mara kwa mara.

“Wakati kama huu uhaba wa maziwa umepunguwa kwa sababu maziwa yako kwa wingi, na kwa sababu sisi tumeanza kuwapatia wakulima ng’ombe tunatarajia kwamba ng’ombe wakianza kuzaa na kukamuliwa lile tatizo la maziwa ambalo tulikuwa tunapata litakuwa haliko”, aliongeza waziri huyo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mradi wa Galana Kulalu kukabili uhaba wa chakula nchini

Published

on

By

Serikali imesema inalenga kufikia ekari 3,200 za kilimo katika mradi wa uzalishaji chakula wa Galana Kulalu ifikapo mwishoni mwa mwaka huu wa 2025.
Waziri wa maji, usafi na kilimo nyunyizi Eric Mugaa alisema tayari ekari 1,060 zimepandwa mahindi kwa kutumia mifumo ya umwagiliaji ya kisasa, mazao ya kwanza yakitarajiwa kuvunwa mwezi Oktoba, huku maandalizi yakuongeza mashamba zaidi yakiendelea.
Akizungumza alipozuru mradi wa Galana Kulalu kutathmini maendeleo ya shughuli za mradi huo, waziri Mugaa pia alisema miundombinu mipya ikiwemo mabwawa ya kuhifadhi maji, mifareji ya kunyunyiza maji, na mitambo ya kusukuma maji imejengwa ilikuwezesha shughuli za unyunyizaji.
Wakati huo huo, waziri huyo alidokeza kuwa ujenzi wa Daraja la Sabaki umefikia hatua ya asilimia 50, akidokezakwamba daraja hilo linatarajiwakukamilika hivi karibuni ili kurahisisha usafirishaji wa vifaa vya kilimo na vile vilekusafirisha mazao kutoka Galana Kulalu.
Serikali kupitia Mamlaka ya unyunyizi iliahidi kuendelea kushirikiana na sekta za kibinafsi kuhakikisha mradi huo wa Galana Kulalu unakuwa suluhu ya uhaba wa chakula hapa nchini.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending