Business
Wakulima 9,500 Kwale Kunufaika na Mavuno Bora Baada ya Kupokea Mbegu za Kisasa

Wakulima zaidi ya 9,500 katika Kaunti ya kwale hasa katika maeneo kame ya Kinango na LungaLunga wanatarajia mavuno zaidi ya mahindi, pojo na kunde, kufuatia serikali ya kaunti hiyo kuwasambazia mbegu za kisasa.
Kupitia idara ya kilimo na ufugaji, wakulima hao wamepokea mbegu hizo pamoja na mbolea ya bei nafuu ili kuendeleza kilimo hasa wakati huu ambapo mvua bado zinaendelea kushuhudiwa maeneo mengi nchini.
Kufikia sasa kaunti hiyo imesambaza tani 206 za mbegu, tani zaidi ya 1,000 za mbolea ya bei nafuu pamoja na matingatinga.
Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza mapato na kuinua uchumi wa eneo hilo.
“Sai tunatarajia mavuno zaidi kufuatia hatua ya serikali ya kaunti kutusaidia na mbegu za kisasa na mbolea ya bei nafuu
Business
Wafanyabiashara Wadogo Kilifi Wakandamizwa na Nauli Ghali

Wafanyibiashara wanaotegemea huduma za tuktuk mjini kilifi kaunti ya kilifi wanalalamikia kukadiria hasara kutokana na hatua ya wahudu hao kupandisha nauli.
Wafanyibaisahara hao ambao ni wa kuhamahama wanasema kuwa hatua ya wahudumu wa tuktuk kuongeza bei ya nauli inawakagandamiza kwani hakuna pesa na kuongeza nauli inafanya maisha kuwa magumu.
Kulingana na wafanyibiashara hao imekuwa vigumu kwa wao kusafiri kutoka soko moja hadi nyingine kuendeleza biashara zao hali ambayo imeathiri maisha yao.
Wametolea wito wahudumu hao kuangizia upya swala hilo ili kuwasaidia wafanyibishara hao kuendeleza shughuli zao kwa urahisi.
Wakati huo huo wameitaka serikali na mamlaka ya udhibiti wa kawi kupunguza bei za mafuta .
Business
Idara ya Vijana Malindi na Magarini Yatishia Hatua Dhidi ya Walioshindwa Kulipa Mikopo

Idara ya vijana eneo bunge la Malindi na Magarini kaunti ya Kilifi inayataka makundi ya vijana, wanawake na walemavu yaliyopata mikopo ya hazina ya uwezo kulipa fedha za mikopo hiyo mara moja ili kuwezesha makundi zaidi kunufaika na hazina hiyo.
Kulingana na afisa msimamizi wa idara hiyo Juma Mtana Mwahunga, asilimia kubwa ya makundi yaliyokopa fedha hizo hayajarudisha hivyo kutatiza utekelezaji wa mpango wa hazina ya uwezo eneo hilo.
Mwahunga amekariri kuwa huenda makundi yaliyochukua mikopo hiyo hayakuzitumia fedha hizo kwa njia mwafaka hivyo kushindwa kulipa mikopo yao kwa wakati unaofaa ili kufanikisha mpango huo.
Afisaa huyo aidha amefichua kuwa jumla ya shilingi milioni 10 za hazina hiyo zilitolewa kupitia mikopo kwa makundi hayo huku milioni 3 pekee zikirudishwa kufikia sasa.