News
Wakristu Waadhimisha Siku ya Ijumaa Kuu

Waumini wa Kanisa Katoliki kote ulimwenguni wamejitokeza kuadhimisha ibada ya njia ya msalaba, wakiashiria ukumbusho wa mateso ambayo Yesu Kristu alipitia kabla ya kufa na kufufuka kulingana na imani ya dini hiyo.
Ibada ya njia ya Msalaba, huadhimishwa kila mwaka baada ya waumuni wa Kanisa Katoliki kukamilisha kipindi cha kufunga na kusali ambayo hutambulika kama Kwaresma, kisha Jumapili ya Matawi na hatimaye kipindi cha Pasaka ambayo huanza rasmi na siku ya Ijumaa Kuu.
Kulingana na Kanisa Katoliki, siku ya Ijumaa kuu, ni kipindi cha mwisho cha maisha ya Yesu Kristu kabla ya kuteswa, kufa na hatimaye kufufuka siku ya tatu ambapo waumuni hao kuadhimisha sherehe za sikukuu ya Pasaka.
Viongozi mbalimbali wa kidini katika Kanisa Katoliki la St Patrick Parokia ya Kilifi wakiongozwa na Padre Marsellous Okello, wamehimiza umuhimu wa unyenyekevu na amani jinsi Yesu Kristu alivyoyaweka maisha yake kwa Mungu.
Hata hivyo maafisa wa usalama wameahidi kuimarishwa kwa usalama katika maeneo mbalimbali ya Pwani ikiwemo maeneo ya burudani, fuo za bahari hindi pamoja na vituo vya kuabiri magari ya uchukuzi wa umma.
News
Macharia: Jamii ya Kilifi kusini watapeliwa ardhi kufuatia ukosefu wa Elimu

Msaidizi wa Kamishna wa kaunti ya Kilifi eneo la Kilifi Kusini, Francis Macharia amesema ukosefu wa elimu umechangia kwa wanajamii wengi kaunti ya Kilifi kutapeliwa katika umiliki wa ardhi.
Akizungumza eneo la Vipingo, Macharia alisema kuwa wanajamii wengi hasa wazee wamekuwa wakitapeliwa mashamba yao kutokana na kukosa kisomo.
Macharia alisisitiza haja ya jamii kuzingatia elimu kwani visa vya ulaghai wa mashamba kutokana na ukosefu wa elimu vimekithiri mno hasa mashanani.
“Kuna baadhi ya vijana pia wamekuwa wakiwatapeli wazazi wao fedha za inua jamii pindi zinapotumwa, na hii imechangiwa na kutosoma wazee hao” aliongeza Macharia.
Macharia alisema wazazi pia wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa wanao wanapata elimu ipasavyo akisema kuwa eneo la Kilifi kusini limekuwa na visa vingi vya watoto wanaoacha shule na kuingilia vibarua.
Taarifa ya Hamis Kombe
News
Makalo atoa wito kwa serikali kuendeleza mpango wa ugavi wa chakula

Mwakilishi wa wadi ya Kasighau kaunti ya Taita Taveta Amos Makalo ametoa wito kwa serikali kuu kuendeleza mpango wa ugavi wa chakula cha msaada katika eneo hilo sawa na maeneo mengine kote nchini ili kunusuru maelfu ya wananchi wanaokabiliwa na baa la nja.
Makalo alisema chakula hicho ni kidogo mno kwani wananchi wengi wa Kasighau pamoja na maeneo mengine ya kaunti hiyo wanakabiliwa na baa la njaa.
Wakati huohuo Makalo alimshinikiza mwakilishi wa kike kwenye kaunti hiyo Lydia Haika kuishawishi serikali kuu kuikumbuka kaunti hiyo katika kupeana misaada mbalimbali ambayo itawafaidi wenyeji.
“Wananchi wanahangaika kutokana na njaa. Na kwasababu umetutembelea na mazuri leo wacha niombe kwamba hayo Mazuri yaendelee kwa muda huu ulio mbele yetu maana hali ni ngumu sana’’
Haya yanajiri huku Serikali ya kitaifa kupitia wizara ya huduma za kitaifa na mipango maalum ikiendeleza shughuli za usambazaji wa chakula cha msaada kwa wahanga wa baa la njaa kaunti ya Taita Taveta na maeneo mengine nchini.
Taarifa ya Janet Mumbi
-
Sports12 hours ago
Harambee Stars Wapiga Ushelisheli Kasarani, Olunga Asawazisha Rekodi ya Oliech
-
News11 hours ago
Viongozi wa jamii ya Mijikenda wakosoa maandazili ya sherehe za Chenda chenda.
-
Sports8 hours ago
Uingereza yawapa wapinzani onyo baada ya kuichapa Serbia 5-0, Haaland apiga mabao matano kwa Norway