News
Wakaazi Waonywa Dhidi ya Kuranda Onyo Katika Fuo za Bahari Hindi

Kamanda wa polisi kaunti ya Kwale Reginald Omaria amewaonya wakaazi dhidi ya kuranda randa ovyo katika fuo za bahari hindi katika masaa yasiokubalika na kwamba atakayepatikana atakabiliwa kisheria.
Omaria anasema kama njia mojawapo ya kuimarisha usalama hakuna mgeni ama mwenyeji anayeruhusiwa kuwa ufuoni baada ya saa kumi na mbili jioni msimu huu wa sherehe ya pasaka.
Kiongozi huyo wa usalama amewataka wazazi kuwalinda watoto wao ili kuwaepusha na visa vya uvunjaji wa sheria.
Kwa upande wake Kamishna wa kaunti ya Kwale Stephen Orinde amesema oparesheni zaidi za kiusalama zinaendelea katika kaunti hiyo.
International News
Iran Yafanya Mashambulizi Qatar

Katika juhudi za kulipiza Mashambulio ya jeshi la Marekani dhidi ya vituo vya Nuklia, Iran Leo Jumatatu Juni 23, imevurumisha makombora na kushambulia kambi ya jeshi la Marekani likuyoko Qatar, Milki za Kiarabu.
Mashambulio hayo ya hivi Punde kabisa katika Mzozo huo wa Mashariki ya Kati, yanazidi wasi wasi katika eneo hilo la Ghuba.
Muda mfupi baada ya shambulio hilo, Bahrain na pia Qatar ambazo ni makao ya kambi ya kikosi Cha 5th Fleet Cha Jeshi la Marekani , zilisitisha mara Moja safari zote za ndege katika anga zao.
Makombora hayo ya Iran yalilenga kambi ya kijeshi ya Al Udeid, nchini Qatar, ingawa jeshi la Marekani liliweza kuyategua makombora hayo kabla ya kusababisha maafa makubwa.
Hakuna habari zozote za majeruhi zilizotolewa kufikia sasa.
Shirika la Habari la AP limeripoti Kwamba, Iran imetoa taarifa kudai kwamba makombora yaliyovurumishwa yanauzani sawa na yale yaliyotumiwa na Jeshi la Marekani kuharibu vituo vyake vya Nuklia huko Fordow.
Hata hiyo lakini, Iran inasema Kwamba ililenga kambi hiyo la Al Ufeid ambayo Iko mbali kidogo na makaazi ya Watu.
Aidha makombora hayo pia yalilenga kambi ya makaazi ya jeshi la Marekani la Ain Al-Assad iliyoko eneo la magharibi mwa Iraq.
Kiongozi wa Iran Ayatollah Ali Khamenei alionya kwamba, Mashambulio hayo ya Marekani yatakuwa na athari kubwa za kiusalama sio tu kwa America bali pia eneo la Mashariki ya Kati.
Mapema Leo Isreal pia ilizidisha Mashambulio yake dhidi ya Iran kulenga gereza ambalo yaaminika limekuwa likitumiwa kuwafungia wanaharakati wa kisiasa nchini humo.
News
Serikali na Wadau wa mazingira wapanda miti, Sabaki

Serikali ya kitaifa kwa ushirikiano na mashirika ya kimazingira kaunti ya Kilifi inaendeleza mpango wa upanzi wa miti ili kuboresha mazingira.
Kulingana na Katibu wa masuala ya vijana na uchumi bunifu nchini Fikirini Jacobs, mpango huo unalenga kurudisha hadhi ya taifa la Kenya katika viwango vya kimazingira.
Akihutubia Wananchi wakati wa zoezi la upanzi wa mikoko katika eneo la Sabaki kaunti ya Kilifi, Fikirini alibainisha kwamba kupitia zoezi hilo jumla ya Miche elfu mbili ya mikoko kutoka kwa serikali na mashirika ya uhifadhi wa Mazingira imepandwa katika eneo hilo.
“Tumepanga miti mingi sana, idara yetu ya vijana imetoa miche elfu na kupitia mashirika mengi hapa wametoa miche elfu kwa jumla tumepanda miti elfu mbili, asante sana kwani kwa kufanya hivyo unasaidia pakubwa”, alisema Fikirini.
Wakati huo huo ameihimiza wananchi kuzingatia suala la upanzi wa miti pamoja na kujiepusha na ukataji miti kiholela, akisisitiza haja ya wakaazi kulinda misitu ili kuiwezesha jamii kuwa mazingira bora.
Taarifa ya Mwanahabari wetu