Connect with us

News

Wakaazi Waonywa Dhidi ya Kuranda Onyo Katika Fuo za Bahari Hindi

Published

on

Kamanda wa polisi kaunti ya Kwale Reginald Omaria amewaonya wakaazi dhidi ya kuranda randa ovyo katika fuo za bahari hindi katika masaa yasiokubalika na kwamba atakayepatikana atakabiliwa kisheria.

Omaria anasema kama njia mojawapo ya kuimarisha usalama hakuna mgeni ama mwenyeji anayeruhusiwa kuwa ufuoni baada ya saa kumi na mbili jioni msimu huu wa sherehe ya pasaka.

Kiongozi huyo wa usalama amewataka wazazi kuwalinda watoto wao ili kuwaepusha na visa vya uvunjaji wa sheria.

Kwa upande wake Kamishna wa kaunti ya Kwale Stephen Orinde amesema oparesheni zaidi za kiusalama zinaendelea katika kaunti hiyo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Macharia: Jamii ya Kilifi kusini watapeliwa ardhi kufuatia ukosefu wa Elimu

Published

on

By

Msaidizi wa Kamishna wa kaunti ya Kilifi eneo la Kilifi Kusini, Francis Macharia amesema ukosefu wa elimu umechangia kwa wanajamii wengi kaunti ya Kilifi kutapeliwa katika umiliki wa ardhi.

Akizungumza eneo la Vipingo, Macharia alisema kuwa wanajamii wengi hasa wazee wamekuwa wakitapeliwa mashamba yao kutokana na kukosa kisomo.

Macharia alisisitiza haja ya jamii kuzingatia elimu kwani visa vya ulaghai wa mashamba kutokana na ukosefu wa elimu vimekithiri mno hasa mashanani.

“Kuna baadhi ya vijana pia wamekuwa wakiwatapeli wazazi wao fedha za inua jamii pindi zinapotumwa, na hii imechangiwa na kutosoma wazee hao” aliongeza Macharia.

Macharia alisema wazazi pia wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa wanao wanapata elimu ipasavyo akisema kuwa eneo la Kilifi kusini limekuwa na visa vingi vya watoto wanaoacha shule na kuingilia vibarua.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

News

Makalo atoa wito kwa serikali kuendeleza mpango wa ugavi wa chakula

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Kasighau kaunti ya Taita Taveta Amos Makalo ametoa wito kwa serikali kuu kuendeleza mpango wa ugavi wa chakula cha msaada katika eneo hilo sawa na maeneo mengine kote nchini ili kunusuru maelfu ya wananchi wanaokabiliwa na baa la nja.

Makalo alisema chakula hicho ni kidogo mno kwani wananchi wengi wa Kasighau pamoja na maeneo mengine ya kaunti hiyo wanakabiliwa na baa la njaa.

Wakati huohuo Makalo alimshinikiza mwakilishi wa kike kwenye kaunti hiyo Lydia Haika kuishawishi serikali kuu kuikumbuka kaunti hiyo katika kupeana misaada mbalimbali ambayo itawafaidi wenyeji.

“Wananchi wanahangaika kutokana na njaa. Na kwasababu umetutembelea na mazuri leo wacha niombe kwamba hayo Mazuri yaendelee kwa muda huu ulio mbele yetu maana hali ni ngumu sana’’

Haya yanajiri huku Serikali ya kitaifa kupitia wizara ya huduma za kitaifa na mipango maalum ikiendeleza shughuli za usambazaji wa chakula cha msaada kwa wahanga wa baa la njaa kaunti ya Taita Taveta na maeneo mengine nchini.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending