Connect with us

News

Wakaazi Waonywa Dhidi ya Kuranda Onyo Katika Fuo za Bahari Hindi

Published

on

Kamanda wa polisi kaunti ya Kwale Reginald Omaria amewaonya wakaazi dhidi ya kuranda randa ovyo katika fuo za bahari hindi katika masaa yasiokubalika na kwamba atakayepatikana atakabiliwa kisheria.

Omaria anasema kama njia mojawapo ya kuimarisha usalama hakuna mgeni ama mwenyeji anayeruhusiwa kuwa ufuoni baada ya saa kumi na mbili jioni msimu huu wa sherehe ya pasaka.

Kiongozi huyo wa usalama amewataka wazazi kuwalinda watoto wao ili kuwaepusha na visa vya uvunjaji wa sheria.

Kwa upande wake Kamishna wa kaunti ya Kwale Stephen Orinde amesema oparesheni zaidi za kiusalama zinaendelea katika kaunti hiyo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mpango wa kuboresha afya ya macho kuanzishwa kaunti ya Mombasa

Published

on

By

Serikali ya Kaunti ya Mombasa kwa ushirikiano na shirika la Christian Blind Mission (CBM) imeanzisha rasmi mpango mpya wa kuboresha afya ya macho kwa wakaazi wa kaunti hiyo.

Kupitia mradi unaojulikana kama Vision Impact, shirika hilo linalenga kupunguza matatizo ya uhafifu wa macho kuona, na upofu unaoweza kuzuilika, kwa kuimarisha huduma za afya na kuongeza uhamasishaji katika jamii.

Mradi huo umefadhiliwa na unatekelezwa katika kaunti saba nchini, huku Mombasa ikiwa miongoni mwao, ukilenga kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu kwa kutambua kuwa ulemavu mara nyingi ni chanzo na pia matokeo ya umasikini.

Mradi huo utajumuisha hamasa kwa jamii na wahudumu wa afya, uchunguzi wa macho shuleni na kwa njia ya kuzuru nyumba hadi nyumba, huku wagonjwa watakaobainika kuwa na matatizo ya kuona wakipewa rufaa kwa matibabu yanayostahili.

Serikali ya Kaunti ya Mombasa iliesema kuwa hiyo ni hatua muhimu katika kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora za afya ya macho na bila ubaguzi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Viongozi wa jamii ya Mijikenda wakosoa maandazili ya sherehe za Chenda chenda.

Published

on

By

Baadhi ya viongozi wa jamii ya mijikenda eneo la pwani wamekosoa mpangilio wa sherehe za kitamaduni za jamii ya kimijikenda maarufu chenda chenda zilizofanyika jana Kaunti za Kilifi na Kwale.

Wakiongozwa na mwenyekiti ya baraza la jamii ya Chonyi Raphael Mwangala walisema msingi wa maandalizi ya sherehe hizo ni mshikamano ya jamii ya Mijikenda na wala sio mgawanyiko kama ilivyoshuhudiwa hapo jana.

Mwangala alisema taswira iliyojitokeza hapo jana hairidhishi kwa wamijikenda na inaonyesha hawana msimamo.

“Walioanzisha hii chenda chenda si lengo la kugawanyana, ni lengo la kuja pamoja, wengine wanachukua tu ni chenda chenda mijikenda waje wakae tu, lakini leo yule anaenda fanya Kwale, yule anaenda fanya wapi, hilo sio lengo, ningewasihi Mijikenda wenzangu, ngewasihi hata viongozi ambao wanajiita ni viongozi wa chenda chenda wafikirie lazima twende pamoja zi mambo ya kugawanyana”, alisema Mwangala.

Anadai sherehe hizo zimeingiliwa kisiasa akisistiza umuhimu wa kubuniwa kamati mpya ya jamii hiyo itakayohusisha mwakilishi wa kila kabila.

“Kwanza kamati ni wakina nani? Ni lazima kamati iuende mpya ya chenda chenda kwa kila mmijikenda awe mule ndani ya kamati ili wakipanga wawe wanaenda pamoja”, aliuliza Mwangala.

Baadhi ya watumbuizaji wa ngoma za kiasili katika sherehe za chenda chenda mjini Kilifi.

Kwa upande wake gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro Mung’aro aliahidi kuunda kamati maalum itakayohusisha wazee wa Kaya ili kuangazia ulinzi wa misitu ya Kaya.

Akizungumza wakati wa sherehe hizo katika chuo kikuu cha Pwani, Gavana Mung’aro alisema kamati hiyo itahakikisha misitu ya kaya inazunghushiwa uwa ili kudhibiti uvamizi wa binadam.

Kauli ya gavana huyo ilijiri baada ya wazee wa Kaya kulalama kuwa misitu ya Kaya imekuwa ikisambaratika kutokana na uvamizi na kutatiza shughuli za mwendelezo wa mila na tamaduni za wamijikenda.

“Nitaunda kamati ya wazee wa Kaya tuangazia maneno ya misitu na mashamba ili kuwekewa ua ili itunzwe dhidi ya wavamizi,tunatengeneza kitengo cha vijana watyakaokuwa walinzi wa msitu kwa sababu tuiko na wizara hiyo ndani ya kaunti”, alisema Mung’aro

Kwa upande wake katibu katika wizara ya vijana na uchumi bunifu Fikirini Jacobs amesistiza jamii ya mijikenda hasa vijana kuzingatia umuhimu majukumu ya  uongozi waliyonayo katika jamii.

Sherehe hizo ambazo ni makala ya nane kufanyika, ilifaa kufanyika kaunti ya Kwale kulingana na mpangilio wa awali wa kufanyika kile eneo la pwani japo kulifanyika mabadiliko siku za mwisho.

Mwenyekiti wa bodi ya barabara nchini Aisha Jumwa na gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani kwenye sherehe za Chenda chenda Kwale

Hatua hiyo ilikashifiwa na baadhi ya viongozi ambapo maandalizi mengine yalifanyika katika msitu wa Kaya Mtswakara kaunti ya Kwale ambapo mwenyekiti ya bodi ya barabara nchini Aisha Jumwa alihudhuria.

Taarifa ya Joseph Jira

 

Continue Reading

Trending