Business
Wafugaji wa Nyuki Lamu Walia Kudorora kwa Biashara ya Asali Kutokana na Asali Ghushi

Wafugaji wa nyuki katika Kaunti ya Lamu wamelalamikia kuporomoka kwa soko la asali halisi, wakilaumu kuongezeka kwa asali ghushi inayojaa sokoni.
Kwa mujibu wa wafugaji hao, baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu wamekuwa wakichanganya sukari kwenye asali na kuiuza kwa bei ya chini, hali inayovuruga ushindani wa haki na kuharibu sifa ya bidhaa ya asali asilia.
Wakizungumza na vyombo vya habari, walisema kuwa biashara yao sasa inaendelea kusambaratika huku wateja wakipungua kwa kasi, wakihofia kununua bidhaa zisizo halisi. Wamekadiria hasara kubwa na kupoteza wateja waliokuwa wa kudumu.
Katika hatua ya kukabiliana na tatizo hilo, mamlaka husika zimeonya kuwa wafanyabiashara wanaouza asali ghushi watachukuliwa hatua kali za kisheria. Wametakiwa kusitisha mara moja biashara hiyo haramu inayowahujumu wakulima halali.
Aidha, wito umetolewa kwa wanunuzi kuwa waangalifu wanaponunua asali, kuhakikisha wanachukua bidhaa kutoka kwa vyanzo vinavyoaminika ili kuepuka kununua bidhaa bandia.
Business
Wafanyabiashara Wadogo Kilifi Wakandamizwa na Nauli Ghali

Wafanyibiashara wanaotegemea huduma za tuktuk mjini kilifi kaunti ya kilifi wanalalamikia kukadiria hasara kutokana na hatua ya wahudu hao kupandisha nauli.
Wafanyibaisahara hao ambao ni wa kuhamahama wanasema kuwa hatua ya wahudumu wa tuktuk kuongeza bei ya nauli inawakagandamiza kwani hakuna pesa na kuongeza nauli inafanya maisha kuwa magumu.
Kulingana na wafanyibiashara hao imekuwa vigumu kwa wao kusafiri kutoka soko moja hadi nyingine kuendeleza biashara zao hali ambayo imeathiri maisha yao.
Wametolea wito wahudumu hao kuangizia upya swala hilo ili kuwasaidia wafanyibishara hao kuendeleza shughuli zao kwa urahisi.
Wakati huo huo wameitaka serikali na mamlaka ya udhibiti wa kawi kupunguza bei za mafuta .
Business
Idara ya Vijana Malindi na Magarini Yatishia Hatua Dhidi ya Walioshindwa Kulipa Mikopo

Idara ya vijana eneo bunge la Malindi na Magarini kaunti ya Kilifi inayataka makundi ya vijana, wanawake na walemavu yaliyopata mikopo ya hazina ya uwezo kulipa fedha za mikopo hiyo mara moja ili kuwezesha makundi zaidi kunufaika na hazina hiyo.
Kulingana na afisa msimamizi wa idara hiyo Juma Mtana Mwahunga, asilimia kubwa ya makundi yaliyokopa fedha hizo hayajarudisha hivyo kutatiza utekelezaji wa mpango wa hazina ya uwezo eneo hilo.
Mwahunga amekariri kuwa huenda makundi yaliyochukua mikopo hiyo hayakuzitumia fedha hizo kwa njia mwafaka hivyo kushindwa kulipa mikopo yao kwa wakati unaofaa ili kufanikisha mpango huo.
Afisaa huyo aidha amefichua kuwa jumla ya shilingi milioni 10 za hazina hiyo zilitolewa kupitia mikopo kwa makundi hayo huku milioni 3 pekee zikirudishwa kufikia sasa.