Connect with us

Business

Wafanyibiashara Malindi Waelezea Kudorora Kwa Utalii Kutokana na Hoteli Kufungwa Eneo Hilo

Published

on

Wafanyibiashara katika sekta ya utalii mjini Malindi kaunti ya Kilifi wameelezea kudorora kwa sekta hiyo kutokana na hatua ya mahoteli mengi eneo hilo kufungwa.

Wakizumguza na vyombo vya habari wafanyiabisha hao wakiongozwa na Boniface Mutuku, wamesema kuwa kufungwa kwa mahoteli kumewasababishia kukadiria hasara kwani kuna bidhaa nyingi ambazo hutumiwa na watalii sasa hivi zinaendelea kuharibika.

Kulingana hali hiyo imesababisha kupungua kwa kiwango kikubwa cha watalii ambao walikuwa wakizuru mji huo hapo awali hivyo kuathiri biashara zao.

Mutuku amemuomba gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro kubuni mbinu za kufufua mahoteli yaliyosambaratika mjini Malindi ambayo yalikua kivutio kikubwa cha utalii eneo hilo ili kuboresha maisha yao.

Aidha ameongeza kuwa kupitia uboreshaji wa maeneo ya utalii na mahoteli nafasi za ajira zitaongezeka na kuboresha maisha ya wakaazi wa eneo hilo na kenya mzima kwa ujumla.

Kwa upande wake Anthony Muasya ambaye pia ni mmoja wa wafanyibiashara hao amewanyoshea kidole cha lawama baadhi ya viongozi mjini Malindi kwa kile anachodai kuwa wameshindwa kuwajibikia suala la kuboresha sekta ya utalii na pia viwanda.

Kulinanga na Muasya viongozi wako na uwezo wa kuboresha utalii na viwanda lakini kufikia sasa hakuna jambo lolote ambalo limefanyika kufikia sasa.

Amewataka viongozi hao kuwajibika ili kuhakikisha kuwa viwanda hivyo vinaimarika ili kuimarisha biashara zao.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

KEMFRI kuanzisha mradi maalum wa kuzalisha mbegu za samaki

Published

on

By

Taasisi ya utafiti wa bahari na uvuvi nchini, KEMFRI, imeanzisha mradi maalum wa kuzalisha mbegu za samaki, ili kuongeza upatikanaji wao na kuinua sekta ya uvuvi nchini.

Akizungumza jijini Mombasa, kaimu mkurugenzi mkuu wa KEMFRI, Dkt. James Mwaluma, alisema kuwa mradi huo unatekelezwa katika eneo la Shimoni kaunti ya Kwale na unalenga kuzalisha samaki wa thamani kubwa kama vile kamba, matiko, na aina nyingine ambazo upatikanaji wake ni nadra.

Dkt. Mwaluma alisema kuwa mbegu zitakazozalishwa kupitia mradi huo zitasambazwa kwa vikundi vya vijana na wanawake wanaojihusisha na shughuli za ufugaji wa samaki, ili kuwawezesha kujitegemea kiuchumi.

Aidha, aliwahimiza vijana kote nchini wakumbatie fursa zilizopo kwenye uchumi wa baharini akisema ni njia mojawapo ya kujikwamua kimaisha na kupambana na ukosefu wa ajira.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

Kaunti ya Kilifi yaendeleza mikakati ya kuimarisha sekta ya uvuvi

Published

on

By

Mkurugenzi wa masuala ya uvuvi kaunti ya Kilifi Mwangi Gachuru amesema serikali ya kaunti ya Kilifi inaendeleza mikakati katika kuimarisha sekta ya uvuvi kwenye kaunti hii ya Kilifi.

Gachuru alisema wanashirikiana na wasimamizi wa fuo za bahari katika kaunti ya Kilifi katika kuhakikisha wavuvi wananufaika kupitia raslimali za baharini.

Aidha, Gachuru aliwahimiza wavuvi na wenyeji wa kaunti ya Kilifi kushirikiana ipasavyo kuhakikisha raslimali hizo zinawafaidi ipasavyo.

“Ni kupitia ushirikiano pekee ndipo mtaweza kuendeleza uvuvi wenu vizuri’’, alisema Gachuru

Akizungumzia mzozo baina ya wavuvi, Gachuru aliwataka kuzingatia sheria zilizopo kwa mujibu wa sheria za uvuvi ili kupatikane mwafaka na sio kuchukua sheria mkononi na kuahidi kuwa watawakabili kisheria wale ambao wanatumia nyavu ambazo zilipigwa marufuku kutumika baharini kuvua samaki.

“Panapotokea ugomvi miongoni mwenu, zingatieni sheria na sio kuchukua sheria mkononi’’ Aliongeza Gichuru.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending