Connect with us

Business

Wafanyibiashara Malindi Waelezea Kudorora Kwa Utalii Kutokana na Hoteli Kufungwa Eneo Hilo

Published

on

Wafanyibiashara katika sekta ya utalii mjini Malindi kaunti ya Kilifi wameelezea kudorora kwa sekta hiyo kutokana na hatua ya mahoteli mengi eneo hilo kufungwa.

Wakizumguza na vyombo vya habari wafanyiabisha hao wakiongozwa na Boniface Mutuku, wamesema kuwa kufungwa kwa mahoteli kumewasababishia kukadiria hasara kwani kuna bidhaa nyingi ambazo hutumiwa na watalii sasa hivi zinaendelea kuharibika.

Kulingana hali hiyo imesababisha kupungua kwa kiwango kikubwa cha watalii ambao walikuwa wakizuru mji huo hapo awali hivyo kuathiri biashara zao.

Mutuku amemuomba gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro kubuni mbinu za kufufua mahoteli yaliyosambaratika mjini Malindi ambayo yalikua kivutio kikubwa cha utalii eneo hilo ili kuboresha maisha yao.

Aidha ameongeza kuwa kupitia uboreshaji wa maeneo ya utalii na mahoteli nafasi za ajira zitaongezeka na kuboresha maisha ya wakaazi wa eneo hilo na kenya mzima kwa ujumla.

Kwa upande wake Anthony Muasya ambaye pia ni mmoja wa wafanyibiashara hao amewanyoshea kidole cha lawama baadhi ya viongozi mjini Malindi kwa kile anachodai kuwa wameshindwa kuwajibikia suala la kuboresha sekta ya utalii na pia viwanda.

Kulinanga na Muasya viongozi wako na uwezo wa kuboresha utalii na viwanda lakini kufikia sasa hakuna jambo lolote ambalo limefanyika kufikia sasa.

Amewataka viongozi hao kuwajibika ili kuhakikisha kuwa viwanda hivyo vinaimarika ili kuimarisha biashara zao.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wafanyabiashara Wadogo Kilifi Wakandamizwa na Nauli Ghali

Published

on

Wafanyibiashara wanaotegemea huduma za tuktuk mjini kilifi kaunti ya kilifi wanalalamikia kukadiria hasara kutokana na hatua ya wahudu hao kupandisha nauli.

Wafanyibaisahara hao ambao ni wa kuhamahama wanasema kuwa hatua ya wahudumu wa tuktuk kuongeza bei ya nauli inawakagandamiza kwani hakuna pesa na kuongeza nauli inafanya maisha kuwa magumu.

Kulingana na wafanyibiashara hao imekuwa vigumu kwa wao kusafiri kutoka soko moja hadi nyingine kuendeleza biashara zao hali ambayo imeathiri maisha yao.

Wametolea wito wahudumu hao kuangizia upya swala hilo ili kuwasaidia wafanyibishara hao kuendeleza shughuli zao kwa urahisi.

Wakati huo huo wameitaka serikali na mamlaka ya udhibiti wa kawi kupunguza bei za mafuta .

Continue Reading

Business

Idara ya Vijana Malindi na Magarini Yatishia Hatua Dhidi ya Walioshindwa Kulipa Mikopo

Published

on

Idara ya vijana eneo bunge la Malindi na Magarini kaunti ya Kilifi inayataka makundi ya vijana, wanawake na walemavu yaliyopata mikopo ya hazina ya uwezo kulipa fedha za mikopo hiyo mara moja ili kuwezesha makundi zaidi kunufaika na hazina hiyo.

Kulingana na afisa msimamizi wa idara hiyo Juma Mtana Mwahunga, asilimia kubwa ya makundi yaliyokopa fedha hizo hayajarudisha hivyo kutatiza utekelezaji wa mpango wa hazina ya uwezo eneo hilo.

Mwahunga amekariri kuwa huenda makundi yaliyochukua mikopo hiyo hayakuzitumia fedha hizo kwa njia mwafaka hivyo kushindwa kulipa mikopo yao kwa wakati unaofaa ili kufanikisha mpango huo.

Afisaa huyo aidha amefichua kuwa jumla ya shilingi milioni 10 za hazina hiyo zilitolewa kupitia mikopo kwa makundi hayo huku milioni 3 pekee zikirudishwa kufikia sasa.

Continue Reading

Trending