Business
Wafanyibiashara Malindi Waelezea Kudorora Kwa Utalii Kutokana na Hoteli Kufungwa Eneo Hilo

Wafanyibiashara katika sekta ya utalii mjini Malindi kaunti ya Kilifi wameelezea kudorora kwa sekta hiyo kutokana na hatua ya mahoteli mengi eneo hilo kufungwa.
Wakizumguza na vyombo vya habari wafanyiabisha hao wakiongozwa na Boniface Mutuku, wamesema kuwa kufungwa kwa mahoteli kumewasababishia kukadiria hasara kwani kuna bidhaa nyingi ambazo hutumiwa na watalii sasa hivi zinaendelea kuharibika.
Kulingana hali hiyo imesababisha kupungua kwa kiwango kikubwa cha watalii ambao walikuwa wakizuru mji huo hapo awali hivyo kuathiri biashara zao.
Mutuku amemuomba gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro kubuni mbinu za kufufua mahoteli yaliyosambaratika mjini Malindi ambayo yalikua kivutio kikubwa cha utalii eneo hilo ili kuboresha maisha yao.
Aidha ameongeza kuwa kupitia uboreshaji wa maeneo ya utalii na mahoteli nafasi za ajira zitaongezeka na kuboresha maisha ya wakaazi wa eneo hilo na kenya mzima kwa ujumla.
Kwa upande wake Anthony Muasya ambaye pia ni mmoja wa wafanyibiashara hao amewanyoshea kidole cha lawama baadhi ya viongozi mjini Malindi kwa kile anachodai kuwa wameshindwa kuwajibikia suala la kuboresha sekta ya utalii na pia viwanda.
Kulinanga na Muasya viongozi wako na uwezo wa kuboresha utalii na viwanda lakini kufikia sasa hakuna jambo lolote ambalo limefanyika kufikia sasa.
Amewataka viongozi hao kuwajibika ili kuhakikisha kuwa viwanda hivyo vinaimarika ili kuimarisha biashara zao.
Business
Kaunti ya Kilifi yaendeleza mikakati ya kuimarisha sekta ya uvuvi

Mkurugenzi wa masuala ya uvuvi kaunti ya Kilifi Mwangi Gachuru amesema serikali ya kaunti ya Kilifi inaendeleza mikakati katika kuimarisha sekta ya uvuvi kwenye kaunti hii ya Kilifi.
Gachuru alisema wanashirikiana na wasimamizi wa fuo za bahari katika kaunti ya Kilifi katika kuhakikisha wavuvi wananufaika kupitia raslimali za baharini.
Aidha, Gachuru aliwahimiza wavuvi na wenyeji wa kaunti ya Kilifi kushirikiana ipasavyo kuhakikisha raslimali hizo zinawafaidi ipasavyo.
“Ni kupitia ushirikiano pekee ndipo mtaweza kuendeleza uvuvi wenu vizuri’’, alisema Gachuru
Akizungumzia mzozo baina ya wavuvi, Gachuru aliwataka kuzingatia sheria zilizopo kwa mujibu wa sheria za uvuvi ili kupatikane mwafaka na sio kuchukua sheria mkononi na kuahidi kuwa watawakabili kisheria wale ambao wanatumia nyavu ambazo zilipigwa marufuku kutumika baharini kuvua samaki.
“Panapotokea ugomvi miongoni mwenu, zingatieni sheria na sio kuchukua sheria mkononi’’ Aliongeza Gichuru.
Taarifa ya Janet Mumbi
Business
Wafanyibiashara wa Shanga wavuna kutokana na watalii Mombasa

Wafanyibiashara kaunti ya Mombasa wanaendelea kuvuna zaidi kutokana na watalii wa ndani na nje waliozuru kaunti hiyo kufuatia maonyesho ya kimataifa ya Kilimo ambayo yalikamilika siku ya Jumapili.
Kulingana na wafanyibiashara wa kuuza shanga eneo la Lights kaunti ya Mombasa walisema idadi ya watalii ambao walitembelea eneo hilo imefanya biashara kuimarika.
Wakizungumza na CocoFm, walisema bei za Shanga zilipanda kutoka shilingi mia tatu hadi mia tano kwa shanga ndogo huku shanga kubwa zikiuzwa kwa shilingi elfu moja
Hata hivyo waliitaka serikali ya kaunti ya Mombasa kuimarisha usalama katika maeneo mengi ya kaunti hiyo ili kuwavutia watalii zaidi.
Taarifa ya Pauline Mwango