Business
Wafanyabiashara Wataka Soko la Matano Mane Kufunguliwa Rasmi

Wito unazidi kutolewa kwa serikali ya kaunti ya kilifi kuhakikisha kuwa soko lililojengwa miaka 15 eneo la Matano mane linafunguliwa ili kuwawezesha kuendeleza biashara zao bila changamoto.
Kulingana na Ngari Kombe ambaye ni moja wa wafanyibiashara eneo hilo shughuli za kibiashara katika eneo hilo ziko chini kwani punde mvua inaponyesha wafanyibiashara wanasusia kwenda sokoni wakihofia bidhaa zao kuharibika.
Akizungumza na meza yetu ya biashara Kombe amesema kuwa kwa sasa wafanyibiashara wanahangaika ili hali kuna soko ambalo wanaweza kuendeleza biashara zao bila changamoto.
Sasa Kombe amewataka viongozi wa eneo hilo kufungua soko hilo rasmi ili kuwawezesha wafanyibiashara kuendeleza shuhuli zao ikizingatiwa kuwa wengi wanategemea biashara kujinua kiuchumi.
“Soko lilijengwa kitambo liko hapo milango imefungwa wafanyibiashara wanahangaika ili hali kuna mahali wanaweza fanyibiashara hapo.
“Tunaomba serikali ya kaunti ifungue hili soko ili wafanyibiashara tusaidike”
Business
Wahudumu wa Uchukuzi Kilifi Walia na Kupanda kwa Bei ya Mafuta

Siku moja baada ya mamlaka ya udhibiti wa kawi nchini, EPPRA kutangaza kupandishwa kwa bei ya mafuta, sekta ya uchukuzi katika kaunti ya Kilifi inaelezea hofu ya kuathirika kwa biashara zao.
Wahudumu wa tuktuk,teksi, bodaboda na magari ya usafiri wa umma hapa mjini Kilifi wanasema kupanda kwa bei ya petrol na diseli kutaathiri pakubwa sekta hiyo ya uchukuzi.
Sasa wanasema kuwa watalazimika kuongeza nauli kwa abiria kutokana na gharama ya mafuta.
Ni hali ambayo imeathiri wakaazi ambao wanatarajiwa kutumia vyombo hivyo vya usafiri wakisema kuwa watalazimika kutembea kwa mguu kwa safari fupi fupi katika utekelezaji wa shughuli zao za kawaida.
Hatahivyo wametoa wito kwa serikali kuhakikisha kuwa inaingilia kati ili kuona kwamba bei za mafuta zinadhibitiwa.
Haya yamejiri huku lita moja ya mafuta aina ya petrol kaunti ya KIlifi ikiuzwa kwa shilingi 183.88 huku diseli ikiuzwa kwa shilingi 169.16 kila lita.
Lita moja ya mafuta ya taa inauzwa kwa shilingi 153.29.
Business
Uhusiano wa Kibiashara kati ya Kenya na Ufaransa Waonyesha Ukuaji Chanya

Takwimu za kibiashara kati ya kenya na ufaransa katika kipindi cha miezi mitatu ya mwisho wa mwaka 2024 zinaonyesha kuwa ufaransa ilileta humu nchini bidhaa za thamani ya shilingi bilioni 6.5 na kuagiza bidhaa za thamani ya shilingi bilioni 5.7 kutoka humu nchini hali iliyoleta uwiano bora wa kibiashara kati ya nchi hizi mbili.
Nchi hiyo sasa inalenga kuimarisha zaidi uhusiano wake na kenya ambapo kenya imewaalika waekezaji zaidi kutoka nchini ufaransa kuekeza katika sekta kadhaa za kenya.
Waziri mwenye mamlaka makuu Msalia Mdavadi anasema ufaransa inalenga sekta za kawi, miundomsingi na tekinolojia ili kuongeza biashara kati yake na kenya.