Connect with us

News

Wadau wa amani wabuni mbinu za kudhibiti utovu wa usalama

Published

on

Wadau wa amani katika kaunti ya Kilifi wameishinikiza jamii kuzingatia amani na uwiano.

Wakiongozwa na Harold Mwatua ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ya amani katika kaunti ya Kilifi, wadau hao walisisitiza haja ya uhusiano mwema baina ya maafisa wa usalama na jamii.

Mwatua alisema hali hiyo itasaidia sana katika kuimarisha usalama katika kaunti ya Kilifi kwa jumla.

“Nyinyi kama jamii mnawafahamu wale wote wanaotekeleza uhalifu, ushirikiano wenu na maafisa wa polisi utawezesha wahalifu kukamatwa na kushtakiwa” alisema Mwatua katika hafla ya kujenga uhusiano mwema baina ya maafisa wa usalama na raia kwenye uwanja wa Karisa Maitha mjini Kilifi.

“Polisi ni binadamu kama wewe, ni mtu kama wewe, ni jirani na ndugu yako tuishi nao kwa amani na uwiano” aliongeza Mwatua.

Akiunga mkono kauli hiyo Mwenyekiti wa baraza la Wahubiri na Maimam ukanda wa Pwani CICC, Askofu Amos Lewa aliataka wakaazi kutojenga uadui na maafisa wa polisi iwapo wanapania kuona utovu wa usalama ukidhibitiwa.

Askofu Lewa pia aliwashinikiza wananchi kuzingatia amani hata katika kupigania haki huku akikashifu vikali maandamano ya vurugu na ghasia yaliyoshuhudiwa siku ya sabasaba jijini Nairobi.

Hafla hiyo iliwaleta pamoja maafisa wa usalama, maafisa tawala, mashirika ya kijamii na wananchi ili kutangaza Amani sawa na kujenga uhusiano mwema kati ya polisi na wananchi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wahudumu wa afya Lamu watishia kuishtaki serikali ya kaunti hiyo

Published

on

By

Wahudumu wa Afya kaunti ya Lamu wametishia kuelekea Mahakamani kuishtaki serikali ya kaunti hiyo kwa kukaidi kutekeleza matakwa yao.

Wahudumu hao waliishtumu serikali ya kaunti ya Lamu kwa kupuuza matakwa yao na badala yake kutumia vitisho ili kuwashurutisha kurejea kazini.

Kulingana na viongozi wa wahudumu hao, licha ya mgomo wao kuendelea kwa zaidi ya wiki mbili serikali ya kaunti hiyo imekataa kata kuandaa vikao vya kusuluhisha malalamishi yao.

Baadhi ya changamoto wanazolalamikia ni pamoja na kufanya kazi kwa zaidi ya miaka 10 bila ya kupandishwa vyeo, kupuuzwa kwa mkataba wa makubaliano ya nyongeza ya mishahara, kunyimwa kwa mishahara kwa baadhi ya wahudumu hao miongoni mwa matakwa mengine.

“Mkiendelea kutufinyilia itabidi tufuate njia ya sheria kwa sababu tunajua tunalilia haki yetu, haiwezekani serikali ya kaunti inashindwa kutupandisha vyeo ilhali tumefanya kazi kwa miaka 15 sasa, hatuwezi kuendelea kufanya kazi katika mazingira duni na pia mkataba wa makubaliano kuhusu nyongeza ya mishahara sharti itekelezwe” walisisitiza viongozi hao.

Wakati uo huo serikali ya kaunti ya Lamu imejibu malimishi yao kupitia barua na kutangaza kuwa mgomu huo ni kinyume cha seria na kuwataka wahudumu hao kurejea kazini mara moja.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

News

Rais Ruto atuma KDF kusimamia ujenzi wa hospitali nchini

Published

on

By

Rais William Ruto ametuma jeshi la KDF kusimamia ujenzi wa vituo vya afya zaidi ya 75 kote nchini katika juhudi za kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa haraka.

Akizungumza katika kaunti ya Narok wakati wa uzinduzi wa hospitali ya Sogoo Level 4, waziri wa ulinzi Patrick Mariru alifichua kuwa ujenzi wa hospitali hiyo yenye mamlaka kamili itakamilika baada ya mda wa miezi 11.

Ujenzi wa hospitali ya Sogoo Level 4 ulivutia rais Ruto alipozuru eneo hilo mwezi mei mwaka 2025, jambo lililomfanya kuagiza KDF kuipandisha hadhi.

Mariru hata hivyo alishikilia kuwa wafanyikazi wote wasio na ujuzi watatolewa kutoka kwa jamii.

“Jeshi litamsimamia mkandarasi. Hilo liwe wazi, kazi yote itafanywa na vijana wa Sogoo. Tutaweka maafisa wawili na kila jioni watanipa ripoti ya maendeleo,” alisema Mariru.

“Tuna zaidi ya miradi 75 tunayosimamia na sio kwamba tunabadilisha wakala wa serikali tunataka tu kushirikiana na ofisi tofauti miongoni mwao wizara za afya na michezo.”

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending