Connect with us

News

Wachungaji 85 Adu, Kilifi wapokea mafunzo ya kukabili itikadi kali

Published

on

Jumla ya wachungaji 85 kutoka wadi ya Adu eneo bunge la Magarini kaunti ya kilifi wanaendelea kupokea mafunzo ya kidini kuhusu sheria zinazoambatana na utoaji wa mafunzo ya dini katika makanisa.

Wakiongozwa na Johnson Kaingu mchungaji wa kanisa la PGM Ramada, wachungaji hao walisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia pakubwa kudhibiti makanisa yanayoendeleza mafunzo ya imani potofu.

Wachungaji hao aidha walipongeza mpango huo wakisema utatoa mwelekeo wa jinsi wachungaji wanavyostahili kuhudumu pasi na kupotosha waumini.

“Tuliposikia habari zile za Shakahola tuliona si vizuri tubaki hivyo ila tupate mafundisho maalum kama wachungaji, ili tuweze kudhibiti makanisa yetu yasiangukie mtego ule wa Shakahola. Ufahamu huu ambao umeletwa huku kwetu Adu umetufanya sisi tutakuwa hata tukisimama tutakuwa hata tukisimama tunajua tunafundisha nini ili watu wa Mungu tujue tutawaelekeza katika njia ambayo inafaa”,walisema wachungaji.

Kwa upande wake Elizabeth Dama mmoja wa wachungaji hao ameupongeza mpango huo akisema utawasaidia kutoa mafunzo ya kweli kwa waumini.

“Tuko wachungaji 85 kupitia Christian Pass ambao wametushika mkono ndio wanatufadhili tufundishwe ndio wanalipa walimu”,alisema mchungaji Dama.

Mafunzo hayo yanayofadhiliwa na shirika la Christian Pass yanajiri baada ya kushuhudiwa kwa idadi kubwa ya maafa ya watu katika msitu wa Shakahola sawa na eneo la Kwa Binzaro kupitia mafunzo ya dini potofu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mackenzie yuko salama, wasema maafisa gerezani Shimo la tewa

Published

on

By

Afisa anayesimamia gereza la Shimo la Tewa, Abdi Willy Adan amekanusha madai yalioibuliwa na mhubiri tata Paul Mackenzie kwamba maisha yake yako hatarini akiwa katika gerezani hilo.

Akizungumza mbele ya mahakama ya watoto ya Tononoka, Adan alisema hakuna vitu vya kutiliwa shaka vilivyowekwa kwenye chumba cha Mackenzie katika gereza hilo la Shimo la Tewa, na kwamba usalama wa gereza uko imara.

Mackenzie, anayekabiliwa na mashtaka yanayohusiana na mauaji ya Shakahola, alikuwa ameomba kuhamishwa hadi Gereza la Manyani lakini Adan alikataa, akisema uzito wa mashtaka unahitaji asalie katika gereza la usalama wa juu.

Adan Pia alisema madai ya Mackenzie ya mgomo wa njaa hayana msingi wowote kwani rekodi zinaonyesha wazi kwamba yeye na washukiwa wengine wanaendelea kula chakula wakiwa gerezani.

Upande wa mashtaka ukiongozwa na Jami Yamina, ulipinga ombi la kuahirisha kwa kesi hiyo kwa sababu ya mgomo wa njaa, na kuutaja kama jaribio la kuchelewesha haki ya waathiriwa.

Hata hivyo Hakimu Nelly Chepchirchir alikataa ombi la kuahirisha kwa kesi hiyo, akisema mgomo wa njaa wa kujiletea sio sababu ya kusimamisha kesi, na akaagiza washukiwa wapewe nafasi ya kuwasiliana na mawakili wao.

Mackenzie na wenzake 34 wanakabiliwa na mashtaka ya mauaji ya watoto katika msitu wa Shakahola kaunti ya Kilifi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Jamii ya Digo kaunti ya Kwale yakosoa serikali kuhusu MRC

Published

on

By

Jamii ya wadigo katika kaunti ya Kwale imejitokeza na kuikosoa serikali dhidi ya kauli yake kwamba kuna tetesi za kuzuka kwa vuguvugu la Mombasa Repubilican Council MRC.

Jamii hiyo ikiongozwa na Balozi Chirau Ali Mwakwere ilisema kauli hiyo ya serikali inalenga kuchangia uzushi na wasiwasi kwa jamii hiyo, kwani kuna njama za kuzuka kwa vuguvugu la MRC.

Balozi Mwakwere, alisema jamii ya wadigo haiungi mkono vuguvugu la MRC na iwapo serikali iko na taarifa zozote kuhusu kauli hizo basi iwaeleze wananchi ili wafahamu na wala sio kuchangia uzushi na wasiwasi kwani kauli hizo huenda zikaathiri sekta ya utalii.

“Tulishangaa kabisa kusikia serikali ikisema hivyo kwa sababu huo ni uzushi na imetutia wasiwasi sana kwenye familia zetu, watoto wetu, sisi wazee, wake kwa waume, kwa sababu hakuna MRC hiyo iliisha zamani, sasa serikali inasema imeanza tena, twaiomba serikali itwambie imeanza tena ni akina nani?”,aliuliza Mwakwere.

Jamii hiyo hata hivyo iliweka wazi kwamba haitakubali kuhusishwa na makundi ambayo hayana msingi wowote kwa wananchi.

“Mwataka kutwambai sisi wanawake wa Kidigo twazaa visirani? Sisi hatujazaa visirani, ielekeweke hivyo hatujazaa na wala hatutazaa visirani. Sisi kama kama magen z wa hapa ndani ya Kwale hatukufanya vurugu la aina yeyote leo tunakuaje sisi ni MRC au kwa sababu sisi niwanyonge?”,walisema wakaazi hao.

Kauli zao zilijiri baada ya serikali kupitia kaunti ya kamishna wa kaunti ya Kwale Stephen Orinde kusema kwamba kuna taarifa za kijasusi za kuchipuka kwa vuguvugu la kundi la MRC ambalo linalenga kutatizo usalama wa kaunti ya Kwale.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending