Connect with us

News

Viongozi wa upinzani waendelea kuisuta serikali

Published

on

Viongozi wa upinzani wameikosoa serikali kwa kukosa kutekeleza ahadi walizotoa kwa wananchi hasa katika kufufua miradi ya kiuchumi nchini.

Wakiungumza katika kaunti ya Kakamega viongozi hao wakiongozwa na kinara wa Chama cha DCP Rigathi Gachagua waliomba wakaazi kushirikiana na kuiondoa serikali katika uchaguzi mkuu ujao.

Viongozi hao walimshtumu Rais William Ruto pamoja na kinara wa chama cha ODM Raila Odinga kwa kile walichosema ni kuwatelekeza wakaazi wa ukanda wa magharibi kila msimu wa baada ya uchaguzi mkuu.

“Nyinyi mnampatia kura anatoa fujo, anaitwa, anaingia kwa serikali anawaacha nyinyi kwa mataa, sasa mimi nimefukuza Ruto kule kwa mlima, nimefunga mlima kifunguo iko hapa kwa gari”,alisema Gachagua.

Kwa upande wake kinara wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka alieleza matumaini ya ushirikiano wao na Gachagua, akisema wanaamini wakipata uungwaji mkono wa wananchi wanambandua rais Ruto mamlakani.

Viongozi hao wanasema serikali imeshindwa kudhibiti taifa hasa kupunguza gharama ya maisha na kutimiza ahadi ya miradi ya maendeleo ya kufaidi mahasla.

“Sisi tumekosana na William Ruto kwa sababu ule mkataba ambao tuliandishana naye kama watui wa mkoa wa magharibi amekataa”,alisema Cleophas Malala.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mabadiliko ya tabianchi yatajwa kuchangia mapato duni ya samaki, Lamu

Published

on

By

Wadau katika sekta ya mazingira kaunti ya Lamu wanasema mabadiliko ya hali ya anga yanayoshuhudiwa sawa na ujenzi wa bandari ya Lamu kumechangia mapato ya samaki kupungua katika bahari hindi.

Mahmoud Yusuf ambaye ni mwanazingira alisema zana za kizamani wanazotumia wavuvi kuvua samaki pia zinachangia mapato duni ya samaki.

Yusuf alisema tangu ujenzi huo wa bandari uanze, maji ya bahari chini yamekuwa na matope kutokana na kuchimbwa na kufukuliwa kwa bahari, hali iliyochangia samaki kutorokea bahari kuu.

Mwanamazingira huyo aliitaka serikali kuwapa wavuvi vifaa vya kisasa vya uvuvi sawa na meli za uvuvi zitakazowawezesha kufika maji makuu, baada ya bandari ya ndani kuharibika.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Gachagua atangaza azma ya kuwania urais 2027

Published

on

By

Kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua ametangaza nia ya kuwania wadhfa wa urais mwaka 2027 akilenga kumg’oa rais William Ruto mamlakani.

Gachagua amekuwa akifanya ziara katika eneo la mlima kenya pamoja na viongozi wa chama chake akitumia mikutano ya barabarani kutangaza azma yake ya kuwania urais.

Kulingana na Gachagua serikali ya sasa inatumia mikutano ya ikulu kuendeleza vitendo vya ufisadi, na ameahidi kuwa akichaguliwa atakomesha matumizi mabaya ya fedha za umma.

Katika ziara hiyo viongozi wa chama chake walieza kuwa Gachagua ndiye mgombea anayefaa kupeperusha bendera ya upinzani, wakidai eneo la mlima kenya limejiondoa katika uungwaji mkono wa serikali ya sasa.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

Trending