Connect with us

Sports

Vilabu Vya KCB Na GSU Mabingwa Taji La Kenya Cup

Published

on

Kilabu ya wanabenki KCB ya wanawake ndiyo mabingwa wa Voliboli taji mpya la Kenya Cup fainali iliopigwa ugani Kasarani Indoor Arena wikendi hii.

Hii ni baada ya vipusa hao wa kocha Japheth Munala kuwashinda Kenya Pipeline kwa seti 3-0 za 25-16,25-19,25-22 katika fainali kali ilipigwa katika uga huo

Kwa mujibu wa kocha huyo ni kwamba haikua mechi rahisi kwao na mabingwa wa taji la ligi ya Voliboli nchini Kenya Pipeline ila walikua wamejipanga vizuri kwa mechi hiyo kuliko mechi yoyote ile.

“Tunaheshimu sana wapinzani wetu,ila niliambiwa wachezaji wangu wamejitoe zaidi kwani nilijua si mechi rahisi dhidi ya Pipeline kwani ni timu nzuri mno.”

Katika upande wa wanaume kilabu ya GSU ilinyuka WanaKDF seti 3-0 za 25-22,26-24,25-17 na kuibukia mabingwa wa kombe hilo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Mabondia Kutoka Vilabu Mbalimbali Nchini, Kuzindua Uhasama Mjini Mombasa

Published

on

By

Zaidi ya mabondia 180 wa kiwango cha juu kutoka vilabu 26 kote nchini wanatarajiwa kushiriki mashindano ya ndondi ya mzunguko wa pili Kenya yanayotarajiwa kuanza hii leo hadi 19 mwaka huu yatakayoandaliwa katika taasisi ya Alliance Francaise jijini Mombasa.

Miongoni mwa mabondia watakaoshiri mashindano hayo ni Bonface Mogunde wa huduma ya polisi nchini ambaye hajapoteza pambano katika uzani wake, mshindi wa dhahabu kwenye Michezo ya Afrika Edwin Okongo wa KDF mabondia wa Mombasa, Kombo Mwinyifaki na Shaffi Bakari, pia watapanda ulingoni.

Mashindano hayo yameandaliwa na chama cha Ndondi cha Kaunti ya Mombasa kwa ushirikiano na taasisi ya Alliance Française kama sehemu ya mradi wa ushirikiano wa michezo kati ya Kenya na Ufaransa uitwao Ndondi Mashinani, kwa usaidizi wa Ubalozi wa Ufaransa.

Michuano hiyo inalenga kukuza vipaji, hasa kwa wanawake na vijana, pamoja na kuandaa wawakilishi wa Mombasa kwa mashindano ya Olimpiki yajayo.

Continue Reading

Sports

Kiungo Wa Junior Stars Aldrine Kibet Ni Mali Ya Celta Vigo

Published

on

By

 Nyota wa timu ya Taifa  ya soka Harambee Stars vijana Chipukizi ‘Junior Stars’  Aldrine Kibet sasa amejiunga rasmi na kilabu ya  Celta Vigo nchini Uhispania.
Hii ni baada ya kutia Saini mkataba na klabu hiyo inayomueka Uhispania kwa misimu minne.
Kiungo huyo wa Junior Stars, ametangazwa rasmi kujiunga na Klabu hiyo  ya Celta Vigo  kwa mkataba wa miaka minne  hadi mwaka 2029.
Kibet mwenye umri wa miaka 19 anajiunga na klabu hiyo baada ya kupitia mafunzo ya mchezo wa kandanda katika Akademia ya Nasty Sports nchini Uhispania  alichojiunga nacho miaka miwili iliopita, punde tu alipomaliza masomo  yake katika shule ya Upili Ya St. Anthony Kitale nchini Kenya.
Mchezaji huyo pia amechezea Junior Stars katika mashindano ya CECAFA humu nchini na Tanzania mwaka jana na mwaka 2023 na pia kombe la bara Afrika kwa Chipukizi mwezi Mei mjini Cairo Misri.
Continue Reading

Trending