Connect with us

Sports

Vilabu Vya KCB Na GSU Mabingwa Taji La Kenya Cup

Published

on

Kilabu ya wanabenki KCB ya wanawake ndiyo mabingwa wa Voliboli taji mpya la Kenya Cup fainali iliopigwa ugani Kasarani Indoor Arena wikendi hii.

Hii ni baada ya vipusa hao wa kocha Japheth Munala kuwashinda Kenya Pipeline kwa seti 3-0 za 25-16,25-19,25-22 katika fainali kali ilipigwa katika uga huo

Kwa mujibu wa kocha huyo ni kwamba haikua mechi rahisi kwao na mabingwa wa taji la ligi ya Voliboli nchini Kenya Pipeline ila walikua wamejipanga vizuri kwa mechi hiyo kuliko mechi yoyote ile.

“Tunaheshimu sana wapinzani wetu,ila niliambiwa wachezaji wangu wamejitoe zaidi kwani nilijua si mechi rahisi dhidi ya Pipeline kwani ni timu nzuri mno.”

Katika upande wa wanaume kilabu ya GSU ilinyuka WanaKDF seti 3-0 za 25-22,26-24,25-17 na kuibukia mabingwa wa kombe hilo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Rais Ruto Awapa Morale Kikosi Cha Stars Kambini

Published

on

By

Rais William Samoei Ruto mapema Leo ametembelea kikosi Cha timu ya Taifa Mpira wa Soka Harambee Stars Ugani Kasarani wanapofanyia mazoezi kwa Kombe la Chan 2025 mwezi ujao.
Hii ikiwa ni njia moja wapo ya kuwapa mortisha vijana wa nyumbani akiahidi Stars nchi nzima iko nyuma Yao.

Ruto amewatakia heri Stars na kuambia vijana wa nyumbani watapata sapoti yoyote wanayohitaji kutoka kwake wanapo peperusha bendera ya taifa hili kwenye kipute cha CHAN mwezi ujao.

“Nataka tushinde kombe hili katika nchi yetu,kila Mkenya yuko nyuma yenu kuwapiga jeki ili mpate matokeo chanya mimi na serikali yangu tunahidi kuwapa sapoti yote kwa kombe hili.”

Rais aliandamana na Waziri wa Michezo Salim Mvurya pamoja na waziri wa Ulinzi Soipan Tuya.

Vijana wa nyumbani wanafungua kampeini Agosti 3 dhidi ya DR. Congo ugani Kasarani ambapo watapiga mechi zao zote.

Continue Reading

Sports

Kasarani Na Nyayo:Uwezo Wa Kubeba Mashabiki Yapungua

Published

on

By

CHAN Siku 17 zimesalia kipute hicho kungoa nanga nchi za Kenya,Uganda na Tanzania.

Serikali ya Kenya kupitia Wizara ya Michezo imetumia Kima Cha zaidi ya Shilingi Bilioni 6.7 kufanyia Ukarabati uwanja wa Kasarani na Shilingi nyingine Bilioni 1.1 Uga wa Nyayo.

Uwanja wa Kasarani Ulifungwa mwaka 2023 Kwa shughuli hiyo ya ukarabati huku uga wa Nyayo ukifungwa mwaka mmoja badaye 2024 kwa Maandalizi ya kipute cha CHAN kinachotarajiwa kung’oa nanga chini ya siku 17 zijazo.
Viwanja hivyo sasa vinauwezo wa kubeba mashabiki 55,000 na 22,000 mtawalia.
Ikumbukwe kabila ya ukarabati wa uwanja wa Kasarani ulikuwa na uwezo wa kuwabeba takriban mashabiki 60,000 huku uwanja wa Nyayo ukibeba mashabiki 30,000.
Continue Reading

Trending