Connect with us

Sports

Vilabu Vinavyoshriki Mashindano Ya CAF Kuvuna Maradufu

Published

on

Ni Afueni kwa vilabu vya Kenya Police na Nairobi United vinavyowakilisha nchi kwenye mashindano ya kilabu bingwa barani  (CAF Champions Ligi) na taji la mashirikisho (CAF Confederation) mtawalia.

Hii ni baada ya shirikisho la soka Barani Afrika CAF kutangaza ongezeko la asilimia 100 ya kipato ambacho vilabu vilikua vinavuna misimu ya nyuma.

vilabu vyote 130 vinatarajiwa kunufaika na ongezeko hilo ambapo vilabu ambavyo vilipokea dolla 50,000 sawa na shilingi milioni 6.4 na ya Kenya sasa vitapokea Dolla Milioni 100,000 sawa na Milioni 12.4 ya Kenya.

Hatua hii mpya iliotangazwa na Rais wa CAF Patrice Motsepe itasaidia pakubwa vilabu katika usafiri na maandalizi kwa ajili ya mashindano hayo kwa jumla.

Kenya inawakilishwa na kenya Police Ligi ya Mabingwa Barani huku Nairobi United wakilisha katika taji la mashirikisho Barani Afrika.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Harambee Stars Kundi La Kifo Kundi B.   

Published

on

By

Huku zikiwa zimesalia siku 15 pekee kung’oa nanga kwa kipute cha CHAN mwezi ujao,
Kenya imeratibiwa kupambana na DRC, Morocco, na Angola katika Kundi A linalotajwa kuwa ndio kundi gumu zaidi yaani Kundi la Kifo.
KUNDI B
Ni Taifa jirani la Tanzania, Burkina Faso, Madagascar na Jamhuri ya Africa ya Kati.
KUNDI C
Uganda itachuana na Algeria,Africa Kusini,Guinea na Nigeria.
KUNDI D:
Congo itakabana koo na Nigeria,Senegal na Sudan Kusini.
 Mechi hizi zitasakatwa katika nyuga za katika Kenya, Uganda na Tanzania,
Continue Reading

Sports

Kiungo Wa Brenford Bryan Mbeumo Sasa Ni Mali Ya United

Published

on

By

Baada ya vute ni kuvute ambayo imedumu kwa kipindi cha mwezi mmoja ni rasmi kwamba kilabu ya manchester United na Brenford wameafikia makubaliano ya pauni milioni 70 ya kiungo mshambulizi Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.

Haya yanajiri baada ya ofa mara mbili ya united kukataliwa na kilabu hio kabila ya kutuma ofa ya mwisho ya pauni milioni 65 na nyongesa ya pauni milioni 5.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano baada kukubali matakwa yake binafsi.

Mbeumo anakua sajili wa pili kwa kocha mkuu Ruben Amorim baada ya ujio wa mshmabulizi Matheus Cunha.

Continue Reading

Trending