Sports
Vilabu Vinavyoshriki Mashindano Ya CAF Kuvuna Maradufu

Ni Afueni kwa vilabu vya Kenya Police na Nairobi United vinavyowakilisha nchi kwenye mashindano ya kilabu bingwa barani (CAF Champions Ligi) na taji la mashirikisho (CAF Confederation) mtawalia.
Hii ni baada ya shirikisho la soka Barani Afrika CAF kutangaza ongezeko la asilimia 100 ya kipato ambacho vilabu vilikua vinavuna misimu ya nyuma.
vilabu vyote 130 vinatarajiwa kunufaika na ongezeko hilo ambapo vilabu ambavyo vilipokea dolla 50,000 sawa na shilingi milioni 6.4 na ya Kenya sasa vitapokea Dolla Milioni 100,000 sawa na Milioni 12.4 ya Kenya.
Hatua hii mpya iliotangazwa na Rais wa CAF Patrice Motsepe itasaidia pakubwa vilabu katika usafiri na maandalizi kwa ajili ya mashindano hayo kwa jumla.
Kenya inawakilishwa na kenya Police Ligi ya Mabingwa Barani huku Nairobi United wakilisha katika taji la mashirikisho Barani Afrika.
Sports
Harambee Stars Kundi La Kifo Kundi B.

Sports
Kiungo Wa Brenford Bryan Mbeumo Sasa Ni Mali Ya United

Baada ya vute ni kuvute ambayo imedumu kwa kipindi cha mwezi mmoja ni rasmi kwamba kilabu ya manchester United na Brenford wameafikia makubaliano ya pauni milioni 70 ya kiungo mshambulizi Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.
Haya yanajiri baada ya ofa mara mbili ya united kukataliwa na kilabu hio kabila ya kutuma ofa ya mwisho ya pauni milioni 65 na nyongesa ya pauni milioni 5.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano baada kukubali matakwa yake binafsi.
Mbeumo anakua sajili wa pili kwa kocha mkuu Ruben Amorim baada ya ujio wa mshmabulizi Matheus Cunha.