Connect with us

News

Vijana wahimizwa kuepuka mihadarati

Published

on

 

Vijana wamehimizwa kujitenga na matumizi ya dawa za kulevya kutokana na athari zake ambazo zimechangia maisha ya vijana wengi kusambaratika.

Hii ni baada ya Mamlaka ya kukabiliana na mihadarati na vileo haramu nchini Nacada kubaini ongezeko la idadi ya vijana katika uraibu huo.

Akizungumza katika shule ya upili ya wavulana ya Malindi high katika kaunti ya Kilifi, mkurugenzi wa Wakfu wa Smachs-Charlene Ruto alisema vijana wana jukumu kubwa la kuchukua mwongozo wa maisha yao na wala sio kulaumu viongozi.

“Fukuza dawa za kulevya, karibisha mabadiliko, huu ndio ujumbe pekee tuliokuja kuwapa leo, vijana, asilimia 70 ya uongozi unaanza na wewe mwenyewe, tunapenda kuelekeza lawama kwa serikali ni mwalimu au mzazi, lakini kama vijana tuchukue jukumu na mabadiliko yanaanza na sisi wenyewe”,alisema Charlene Ruto.

Kwa upande wake Rais wa Muungano wa wanafunzi kaunti Kilifi Kahindi James Kalama alisema kaunti ya Kilifi ina vijana wengi ambao ni waraibu wa dawa za kulevya jambo ambalo linafaa kuangaziwa kwa kina, kauli ambayo iliungwa mkono na rais wa Jumuiya ya wanafunzi wa Pwani David Msongori.

“Kilifi inaidadi kubwa ya vijana ambao wameathirika na matumizi ya dawa za kulevya, tukifuata takwimu za Nacada na ndio maana tumekuja na kongamano kama hili ambao tuko nalo siku ya leo kuhamasisha athari ya mihadarati ili waweze kuachana nayo na kufuata elimu”, alisema Kalama.

Kwa upande wake naibu gavana wa kaunti ya Kilifi Flora Mbetsa Chibule aliwahimiza wanafunzi kuzingatia masomo yao ili kubadili msimamo wa maisha yao badala ya kujiingiza katika mambo yasiofaa.

“Mbali na kwamba tunafukuza dawa za kulevya eneo letu, nyinyi wanakilifi leo na vijana wote nchini tunasema tunawatambua na serikali inaimani na nyinyi.”, alisema Chibule.

Baadhi ya viongozi wa mashirika walioandamana na mwanawe rais William Ruto walisema matumizi ya dawa za kulevya yamesambaratisha maisha ya vijana wengi ambao wamekosa mwelekeo maishani, wakiwarai viongozi wa kaunti kuweka mikakati ya kunusuru maisha ya vijana hao.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Kanda ya Pwani kuimarika kupitia Kilimo cha kisasa

Published

on

By

Kanda ya Pwani inatarajiwa kuimarika zaidi kupitia Kilimo cha kisasa kinachotekelezwa kupitia mfumo wa teknolojia.

Hii ni kupitia mikakati inayoendelezwa na Agitech Seedlings kuhakikisha Wakulima na Wenyeji wa Kanda ya Pwani wanakumbatia Kilimo cha kisasa kama maeneo mengine nchini.

Akizungumza na Coco FM katika maonyesho ya Kilimo cha kisasa na uzinduzi wa tawi jipya la Agitech Seedling katika eneo la Kwa Ndomo mjini Malindi kaunti ya Kilifi, Mkurugenzi wa Agitech Seedlings Peter Karanja Ndung’u alieleza sababu za kuanzisha Kilimo hicho cha kisasa katika ukanda wa Pwani.

Karanja pia alisema wanapania kuhakikisha wenyeji wa Pwani wanahamasishwa ipasavyo na hata kuonyeshwa namna ya kufanya Kilimo hicho hapa pwani.

“Kupitia hamasa ambazo tunatoa kwa wakulima na wenyeji wa Pwani kwa jumla tunatarajia kuwa Kilimo kitaanza kuimarika na kuondoa dhana ambayo imekuwepo kwamba eneo la Pwani linatambulika pekee kwa masuala ya uvuvi’’, alisema Karanja.

Vilevile, Karanja alisema kuna haja ya Wakulima kutunza ardhi zao kwa kuhakikisha zina rutuba ya kutosha ili kuzalisha chakula kwa wingi na bora.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Kongamano la kukomesha visa vya dhuluma za kijinsia Taita Taveta

Published

on

By

Idara ya usalama kaunti ya Taita taveta imeandaa kongamano maalum ili kujadili namna ya kukomesha visa vya dhuluma za kijinsia na kingono kaunti hiyo.

Kongamano hilo limefanyika katika eneo la Werugha, eneo bunge la Wundanyi kaunti ya Taita Taveta na limejumuisha maafisa wakuu wa serikali ya kaunti hiyo, viongozi wa kijamii pamoja na wananchi.

Kamishna wa kaunti ya Taita Taveta Josephine Onunga alibainisha kuwa kuna ongezeko la visa 186 ndani ya miaka miwili, eneo bunge la Taveta likirekodi visa 64 huku Wundanyi ikirekodi 38 hivyo kuwataka wakaazi kushirikiana na idara mbalimbali za usalama ili kukomesha visa hivyo.

“Tunapendekeza ushirikiano mkubwa zaidi na zaidi kuanzia mashinani kila boma tulindane, tujuliane hali, hakikisha unamlinda mwenzako”, alisema Onunga.

Kwa upande wao Wanaharakati wa kupambana na dhuluma za kijinsia wakiongozwa na Mary Mgola walieleza hofu yao kutokana na ongezeko la visa hivyo hasa maeneo ya mashinani.

Walisema ukosefu wa mashahidi wa kutosha wakati kesi hizo zinapowasilishwa Mahakamani, ikitajwa kama changamoto kuu wakati wa kusuluhisha kesi hizo.

Mgola aliitaka Mahakama kuhakikisha wanatoa ulinzi wa kutosha kwa mashahidi wa kesi za dhuluma za kijinsia na kingono.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

Trending