Entertainment
Verse Smart, Rojo Mo Amsifia Nyota Ndogo

Wimbo mpya wa “BARAKA” unaowakutanisha Rojo Mo, Nyota Ndogo, Chikuzee, na Cannibal The Chosen One unaendelea kumwagiwa sifa kwenye mitandao ya kijamii kwa kukutanisha lejendari wa mziki wa Pwani – si tu kwa beat kali na ujumbe wake wa kusifu Mungu.
Tukio la hivi punde ni Rojo Mo kusifia verse ya Nyota Ndogo kwenye wimbo huo. Rojo Mo, mmoja wa wasanii wenye ushawishi mkubwa katika scene ya muziki, alitoa maneno haya kupitia ukurasa wake wa Facebook:
“Leo ni NYOTA NDOGO Big up kwa verse smart 🌸 Maua yako pokea #BARAKA”
Rojo Mo amekuwa akiachia picha za walioshirikiana kwenye wimbo akiskuma link ya wimbo wao; alianza na Chikuzee na sasa amefika kwa Nyota Ndogo. bila shaka kesho tutaona picha ya Canibal aliyemtakia heri kwenye siku ya kuzaliwa Juni tarehe tatu.
Katika wimbo huu, Nyota Ndogo anaingia akisifia penzi analolipata kutoka kwa Mungu kabla ya Chikuzee kuchukua hatamu. Ushirikiano wa wasanii hawa wanne – Rojo Mo nyota wa hits, Nyota Ndogo mkwasi wa sauti kutoka Mombasa, Chikuzee mwenye uandishi wa kina na sauti ya kipekee, pamoja na Cannibal The Chosen One, mkali wa mtindo huru (freestyle) – umeleta ladha ya kipekee kwenye track hii.
Kando na ubunifu wa kisanaa, wimbo wa BARAKA unajitokeza pia kama aina ya wimbo wa kusifu na kutoa shukrani – sio kwa mtazamo wa kidini pekee, bali wa maisha ya kila siku. Wasanii wote wanne wanaelezea jinsi Mungu anavyowafungulia milango ya baraka na ufanisi. Wanarejesha sifa kwa Mungu kwa matendo yake makuu. Maneno yao yanagusa roho na kutufundisha kuwa kila hatua ya maendeleo si tu baraka inayostahili kusherehekewa bali pia ni fursa ya kumpa Mungu shukurani.
Huu ni wimbo unaotufundisha kuona uzuri hata katika magumu, na kukumbuka kusema “asante” – kwa uhai, kwa familia, kwa kipaji, na hata kwa yale tuliyoyapitia. Kwa namna ya kipekee, BARAKA inakuwa sauti ya sifa, sala ya mitaani, na salaam ya matumaini kwa yeyote anayeisikiliza akiwa kwenye safari yake ya maisha.
Mashabiki mitandaoni wameonyesha mapenzi yao kwa wimbo huu, wakisifia utunzi, video ya kuvutia, na “chemistry” ya wasanii waliokutana. Lakini zaidi.
Katika dunia ya muziki, si kila wimbo ni wa kawaida. Wimbo wa “BARAKA” ni reminder kwamba muziki unaweza kuwa tiba, kuwa nuru, na kuwa silaha.
Entertainment
Penzi Lao Lazaa Matunda: Jux na Priscilla Watarajia Mwana

Binti wa mwigizaji mashuhuri wa Nollywood, Iyabo Ojo, ambaye ni Priscilla Ojo, na mumewe, nyota wa muziki kutoka Tanzania Juma Jux, wametangaza kuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza.
Wapenzi hao walishiriki habari hizo njema kupitia mtandao wa Instagram kwa picha maridadi za ujauzito, ambapo Priscilla alionekana akionyesha tumbo lake la ujauzito. Picha hizo zilifuatana na maandishi mafupi: “Mum & Dad.”
Safari ya kimapenzi ya wawili hao imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu, ikijumuisha harusi kadhaa zilizofanyika nchini Nigeria na Tanzania, hatua ambayo iliangazia muunganiko wa tamaduni zao mbili.
Juma Jux alimvisha pete ya uchumba Priscilla mara mbili, ambapo ombi la pili lilikuwa la kipekee na lisilosahaulika, lililofanyika jijini Lagos, Nigeria.
Wapenzi hao waliadhimisha safari yao ya ndoa kwa sherehe mbalimbali, zikiwemo harusi ya kitamaduni ya Kiyoruba, harusi ya kanisani (white wedding), na sherehe nyingine zilizoandaliwa kwa fahari kubwa mnamo Aprili 17 na 19, zote zikiwa jijini Lagos.
Kadiri wanavyojiandaa kwa ujio wa mtoto wao wa kwanza, pongezi na salamu za heri kutoka kwa mashabiki na jamaa zimekuwa zikitiririka kwa wingi.
Entertainment
Lisemwalo Lipo, Apewe Nafasi Afunguke, Kaa la Moto Amkingia Kifua Kelechi Africana

Msanii nguli wa muziki Afrika Mashariki, Kaa la Moto, amekingia kifua kauli ya msanii mwenzake Kelechi Africana aliyedai kuwa “kinachowafelisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”
Akizungumza na meza ya burudani ya Coco FM, Kaa la Moto alieleza kuwa anaamini nia ya Kelechi si ya kubeza bali ya kutaka kuona mabadiliko chanya kwenye tasnia ya muziki kutoka ukanda wa Pwani.
“Ameona ndio maana anayakemea,” alisema Kaa la Moto kwa utulivu.
“Naamini kwamba ana ufahamu sahihi, na pia naamini kuwa ni kijana ambaye anataka maendeleo ya sanaa kutoka mkoa wake. Kwa hiyo watu walipatie fikra—kwa sababu lisemwalo lipo. Labda ana kitu, akipewa nafasi atazungumza zaidi.”
Kauli ya Kelechi ilizua hisia mseto mitandaoni baada ya kupachikwa kwenye ukurasa wake wa Facebook, ambapo aliandika: “Kinacho felisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”
Wengine waliona ni matusi kwa jumuiya ya wasanii, lakini kwa Kaa la Moto, ilikuwa ni hoja yenye mzizi wa ukweli. Alisisitiza kuwa hakuna hoja inayopaswa kupuuzwa kabla ya kueleweka kwa undani.
“Sipingi hoja yake kwa sababu kila hoja ipo huru kwa aliyeifikiria na kuiwaza. Naamini anajaribu kuinspire vijana wenzake,” aliongeza Kelechi.
Katika mazungumzo hayo, Kaa la Moto pia alitumia fursa hiyo kueleza kinachomuweka relevant kwenye muziki licha ya mabadiliko ya ladha, mitindo, na majina mapya kwenye game kila mwaka.
“Kitu ambacho kimeniweka hadi leo ni nidhamu. Nidhamu kwenye maisha, kwenye kazi, kwenye watu,” alisema kwa msisitizo.
Baadhi ya mashabiki waliopena maoni yao kwenye post ya Kelechi walisema;
Tamara Black, “Shida tu unaingililia watu hawana shughuli yako.Put that effort in Use ututolee kazi kali umbea achia watoto wa kike.”
Raisi Wakitaa, “Apo umenena nimepata mwenzangu sasa wakusema ukweli wanaboesha Sana Kwanza uyo my wife ndo kabisa simuelewi kila siku post ya mtu mmoja demu mwenyewe alishaliwa na wahuni toka enzi za shule .”
D Jay Ricious,”Wapashe adi wagutuke maana tulio chini ni huko juu ndio twaja kwa nafasi zetu. #coast music occupy kenya .”
Hamza Ahmed Lama, “Acha kutafuta Kiki’kai anapiga hela na anamadili kibao.”
Knasty Snaty, “Wew nawew wataka dera kazi yako ni umbea tu acha mziki uanze umbea.”