Connect with us

News

UNICEF: Watoto milioni 138 wanashiriki ajira za utotoni

Published

on

Takriban watoto milioni 138 walishirikishwa katika ajira za watoto kote duniani mwaka 2024.

Kulingana na ripoti mpya iliyotolewa na Shirika la umoja wa mataifa la watoto duniani, UNICEF na Shirika la kimataifa la ajira, ILO ilionyesha wazi kwamba watoto hao walikuwa wakinyanyaswa haki zao za kimsingi.

Idadi hiyo inajumuisha karibu watoto milioni 54 ambao walifanya ajira ambazo huenda zikaathiri afya na usalama wao.

Mkuu wa UNICEF, Christian Schneider alisema Ripoti hiyo pia ilisema visa vya ajira kwa watoto vinafanyika aghalabu katika Kilimo huku mataifa yaliyo chini ya Jangwa la Sahara yakiathirika pakubwa ambapo watoto milioni 87 waliathirika.

“Ripoti mpya ya ajira kwa watoto ilionyesha ukweli mchungu kwamba mamilioni ya watoto bado wananyimwa haki ya kusoma, kucheza na kuwa watoto, licha ya maendeleo yaliyopatikana,” alisema Schneider.

Idadi hiyo lakini ilionyesha kupungua kwa idadi ya watoto wanaoathirika kwani katika kipindi cha kati ya mwaka 2021-2024, idadi ya watoto walioshiriki ajira za utotoni ni 138 ikilinganishwa na mwaka 2016-2020 ambapo watoto milioni 160 waligundulika kufanya kazi.

Licha ya kupungua kwa idadi hiyo, lengo la kuangamiza ajira kwa watoto kufikia mwaka 2025 halitofikiwa kama ilivyoainishwa kwenye malengo ya ustawi ya Umoja wa Mataifa.

Ripoti hiyo ilitolewa kuelekea siku ya kimataifa ya kupinga ajira kwa watoto duniani itakayoadhimishwa siku ya Alhamis.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Published

on

By

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.

Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.

“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi

Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.

Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending