Connect with us

News

UN yakosoa mauaji ya Saba saba

Published

on

Ofisi ya kamishna mkuu wa haki za kibinadamu wa umoja wa mataifa (OHCHR) imeibua wasiwasi kuhusu maandamano ya siku ya Saba Saba nchini Kenya, ambapo makumi ya raia waliuawa na wengine kujeruhiwa.

Katika taarifa yake siku ya Jumanne, kamishna mkuu wa umoja wa mataifa wa haki za kibinadamu Volker Türk alilaani ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Kenya, na kuahidi kushirikiana na Kenya katika kutatua changamoto vile vile katika uchunguzi.

“Tumesikitishwa sana na mauaji ya jana ya takriban watu 10, pamoja na uporaji na uharibifu wa mali nchini Kenya wakati polisi na vikosi vingine vya usalama vilijibu maandamano ya ghasia katika mji mkuu wa Nairobi na kaunti zingine 16. Risasi za sumu, risasi za mpira, gesi ya kutoa machozi na maji ya kuwasha zilitumika,” ilisema OHCHR kupitia msemaji wake Ravina Shamdasani.

Türk alitoa wito wa utulivu pamona na heshima kamili kwa uhuru wa kujieleza, kujumuika na kukusanyika kwa amani.

“Ni muhimu kwamba malalamiko halali katika mzizi wa maandamano haya yashughulikiwe,” alisema.

Kamishna Mkuu pia alihimiza kwamba mauaji na ukiukwaji wa haki za binadamu “kuchunguzwa kwa haraka, kikamilifu, kwa uhuru na kwa uwazi.”

Wakati wa maandamano ya Julai 7, 2025, polisi waliripoti kwamba raia 11 waliuawa na 567 walikamatwa.

Pia, huduma ya kitaifa ya polisi (NPS) ilisema maafisa 52 na raia 11 walijeruhiwa, magari 12 ya polisi, magari 3 ya serikali na magari 4 ya raia yaliharibiwa.

“Chini ya sheria ya kimataifa ya haki za binadamu, nguvu ya kimakusudi ya maafisa wa kutekeleza sheria, ikiwa ni pamoja na silaha, inapaswa kutumika tu inapobidi ili kulinda maisha kutokana na tishio linalokaribia,” aliongeza Türk.

Maandamano yaliyoshuhudiwa siku ya Saba Saba yalikuja baada ya wiki mbili tu baada ya raia 15 kuuawa mnamo Juni 25, 2025.

Kisha, wakenya waliandamana katika ukumbusho wa mauaji ya zaidi ya watu 60 wakati wa maandamano ya kupinga ushuru mnamo Juni 2024.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending