Connect with us

News

UN yakosoa mauaji ya Saba saba

Published

on

Ofisi ya kamishna mkuu wa haki za kibinadamu wa umoja wa mataifa (OHCHR) imeibua wasiwasi kuhusu maandamano ya siku ya Saba Saba nchini Kenya, ambapo makumi ya raia waliuawa na wengine kujeruhiwa.

Katika taarifa yake siku ya Jumanne, kamishna mkuu wa umoja wa mataifa wa haki za kibinadamu Volker Türk alilaani ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Kenya, na kuahidi kushirikiana na Kenya katika kutatua changamoto vile vile katika uchunguzi.

“Tumesikitishwa sana na mauaji ya jana ya takriban watu 10, pamoja na uporaji na uharibifu wa mali nchini Kenya wakati polisi na vikosi vingine vya usalama vilijibu maandamano ya ghasia katika mji mkuu wa Nairobi na kaunti zingine 16. Risasi za sumu, risasi za mpira, gesi ya kutoa machozi na maji ya kuwasha zilitumika,” ilisema OHCHR kupitia msemaji wake Ravina Shamdasani.

Türk alitoa wito wa utulivu pamona na heshima kamili kwa uhuru wa kujieleza, kujumuika na kukusanyika kwa amani.

“Ni muhimu kwamba malalamiko halali katika mzizi wa maandamano haya yashughulikiwe,” alisema.

Kamishna Mkuu pia alihimiza kwamba mauaji na ukiukwaji wa haki za binadamu “kuchunguzwa kwa haraka, kikamilifu, kwa uhuru na kwa uwazi.”

Wakati wa maandamano ya Julai 7, 2025, polisi waliripoti kwamba raia 11 waliuawa na 567 walikamatwa.

Pia, huduma ya kitaifa ya polisi (NPS) ilisema maafisa 52 na raia 11 walijeruhiwa, magari 12 ya polisi, magari 3 ya serikali na magari 4 ya raia yaliharibiwa.

“Chini ya sheria ya kimataifa ya haki za binadamu, nguvu ya kimakusudi ya maafisa wa kutekeleza sheria, ikiwa ni pamoja na silaha, inapaswa kutumika tu inapobidi ili kulinda maisha kutokana na tishio linalokaribia,” aliongeza Türk.

Maandamano yaliyoshuhudiwa siku ya Saba Saba yalikuja baada ya wiki mbili tu baada ya raia 15 kuuawa mnamo Juni 25, 2025.

Kisha, wakenya waliandamana katika ukumbusho wa mauaji ya zaidi ya watu 60 wakati wa maandamano ya kupinga ushuru mnamo Juni 2024.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mvuvi aliyezama baharini Watamu apatikana Tanariver

Published

on

By

Mwili wa mvuvi Hudhefa Laly aliyepotea baharini huko Watamu eneo bunge la Kilifi Kaskazini Kaunti ya Kilifi akiwa na ndugu yake Athman Laly umepatikana eneo la Shakiko -Mathole, kaunti ya Tana River.

Ndugu hao wawili walitoweka habarini siku ya Alhamisi 24, Julai 2025 katika bahari hindi wakati wakiendelea na shughuli zao za uvuvi.

Vitengo mbali mbali vya uokozi vimekuwa vikiendesha zoezi la kutafuta miili ya wawili hao kwa ushirikiano na wavuvi eneo la Watamu.

Kufikia sasa mwili wa Athman Laly kakake Hudhefa ungali haujapatikana huku juhudi za kuutafuta zikiendelea.

Jamii ya wavuvi katika eneo la Watamu ikiongozwa na kiongozi wa vijana Bakari Shaban iliiomba serikali ya kaunti ya Kilifi na ile ya kitaifa kununua boti za uokozi ili kusaidia kuokoa maisha wakati kunapotokea dharura baharini.

“Tunaomba tupate boti za kuokoa maisha baharini, popote alipo waziri Ali Joho angalau tupate boti za uokozi kama mbili hapa Watamu ni kitovu cha utalii kunamahoteli mengi, watalii wote wanaokuja Watamu mpaka leo hakuna boti za uokozi”, alisema Shaban.

Awali wao wazazi wa wavuvi waliopotea baharini Lali Athman Lali na Dhurai Mohamed Ali waliiomba serikali kuweka juhudi zaidi za kuwasaidia kuwapata wanawao kwani ndio tegemeo kubwa kwa familia yao.

“Uko usaidizi unatumika, kuna vijana wanaojitolea kwa maboti wanaenda ile sehemu ambayo wavuvi wanavua, wanajaribu kuzunguka lakini toka siku hiyo hawajapata chochote: Katika Maisha yangu mimi nawategemea hawa watoto kunisomeshea hawa watoto wangu ambao ni wadogo zao mashule, kwa chakula kwa hivyo naomba serikali inisaidie kwa sababu ndio tegemeo langu hao watoto”.walisema wazazi.

Kisa hiki kilijiri miezi kadhaa baada ya mvuvi mmoja kutoka eneo la Mnarani mjini Kilifi kufariki baharini baada ya kugongwa kichwani kwa pondo na wavuvi wenzake kulipotokea mzozo kuhusu pato la samaki.

Kufikia sasa mwili wa mvuvi huyo haujapatikana.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mombasa inaongoza kwa maambukizi ya MPOX nchini

Published

on

By

Wizara ya afya nchini imesema kaunti ya Mombasa inaongoza kwa visa vya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Kwa mujibu wa mkurugenzi mkuu wa idara ya afya nchini Daktari Patrick Amoth, kaunti ya Mombasa imerekodi visa 139 kati ya visa 300 vilivyoripotiwa na wizara hiyo.

Amoth alidokeza kuwa serikali itatangaza siku maalum ya kutoa chanjo ya kudhibiti msambao wa ugonjwa huo wakishirikiana na shirika la afya ulimwenguni WHO.

Mkurugenzi huyo vile vile alimesema zoezi hilo litaambatana na hamasa kwa wananchi kuhusu namna ya kujikinga na maambukizi zaidi.

“Kwa wakati huu Mombasa ndio inaongoza kwa idadi ya visa 139 kwa hivyo tuchuke tahadhari kuhakikisha kwamba tunazuia maambukizi, na tunafanya mpango pamoja na shirika la afya duniani WHO, hapa tutakuja na mpango wa chanjo na ikifika huo wakati tunaomba watu wajitokeze wapate chanjo ili wapate kinga”,alisema Daktari Amoth.

Wakati huo huo Amoth aliokeza kuwa uchunguzi wa vifo vya watu wanne walioaga dunia wiki chache zilizopita huko Migadini, eneo bunge la Changamwe kaunti ya Mombasa umebaini walifariki kutokana na magonjwa mengine na wala sio maambukizi ya ugonjwa wa MPOX kama ilivyodhaniwa na wakaazi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu.

Continue Reading

Trending