Connect with us

News

Uingereza imeekeza dola milioni 60 kwa mradi wa Kawi ya jua, Kilifi

Published

on

Serikali ya Uingereza ilitangaza kuekeza kima cha dola milioni 60 zaidi katika mradi wa uzalishaji wa Kawi ya miale ya jua katika eneo la Langobaya kaunti ya Kilifi.

Kulingana na Balozi wa Uingereza nchini Kenya Neil Wigan, hatua hiyo itasaidia kuongeza viwango vya uzalishaji wa kawi ya miale ya jua katika kituo hicho.

Wigan alidokeza kwamba mpango huo unalenga kuimarisha pakubwa sekta ya uwekezaji nchini hasa katika kaunti ya Kilifi.

“Tumeekeza zaidi ya dola milioni 60 kwa ajali ya kuekeza mradi huu kwani aliyekuwa akijenga mradi huo alikuwa anautekeleza kwa nafasi ndogo lakini vile tumemsaidia itafungua kazi nyingi na tunafikia kuongeza zaidi ili kufikia mega watsi 80”, alisema Wigan.

Kawi ya miale ya jua katika eneo la Langobaya, Malindi

Kauli yake imeungwa mkono na Katibu wa idara ya uekezaji nchini Abubakar Hassan ambaye amesema uzalishaji wa kawi katika kituo hicho ni hatua muhimu kwa taifa la Kenya kwani itasaidia kupunguza bei ya umeme sawa na kulinda mazingira.

Kwa upande wake Naibu Gavana wa kaunti ya Kilifi Flora Mbetsa Chibule amesema kaunti ya Kilifi kupitia uongozi wa Gavana Gedion Mung’aro inathamini sana uungwaji mkono kutoka kwa serikali ya Uingereza na hatua hiyo inaonyesha wazi ushirikiano mwema katika ya serikali ya Kenya na Uingereza.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Published

on

By

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.

Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.

“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi

Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.

Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending