Connect with us

Sports

Thomas Frank Kocha Mpya Spurs!

Published

on

Kilabu ya Tottenham Hotspurs kumtangaza kocha wa sasa wa Brenford Thomas Frank kuwa kocha mpya wa kilabu hiyo kumrithi Ange Postecoglou aliyepigwa kalamu wiki jana kutokana na msururu wa matokeo duni.

Kulingana na mkali wa taarifa Uhamisho barani Ulaya Fabrizio Romano ni kwamba makubaliano ya pande zote mbili zimafikiwa huku Spurs wakiwa tayari kulipia ada ya pauni milioni 10 ikiwa ni kifungu kilichomo kwenye mkataba wa kocha huyo kabila kukamilisha usajili huo.

Duru za kuaminika zaarifu kwamba mwalimu huyo amekubaliana na kilabu hiyo kwa matakwa ya binafsi na yuko tayari kuanza upya na kilabu hiyo ya London Kaskazini msimu ujao.

Raia huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 51 aliongoza Brenford kumaliza kumi bora msimu uliopita na alama 56.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Sane Sasa Ni Mali Ya Galatasaray

Published

on

By

Ni rasmi aliyekua kiungo wa Manchester cityna Bayern Munich ya Ujerumani Leroy Sane amekamilisha uhamisho wake katika kilabu ya Galatasaray ya Uturuki bila ada yoyote.

Sane mwenye umri wa miaka 30 amepasi vipimo vya kimatibabu baada ya kuwasili mjini Istanbul alipolakiwa na mshabiki wengi wa kilabu hiyo anapojiunga na mabingwa hao wa ligi ya Uturuki.

Mchezaji huyo alijiunga na Bayern Munich msimu wa mwaka 2020 akitokea Mancity kwa mkataba wa miaka mitano na amefanikiwa kufunga magoli 61 katika mechi 220 ambazo amechezea timu hio.

Kiungo huyo pia amekua nguzo muhimu kwa timu ya taifa la Ujerumani akifanikiwa kufunga magoli 14 katika mechi 70 ambazo ameshirikisha katika timu hiyo.

Sane ni miongoni mwa wachezaji walionyeshwa mlango na kilabu ya Bayern Munich kwa msimu mpya.

Continue Reading

Sports

Harambee Starlets Kuelekea TZ Kwa Mechi Za CECAFA

Published

on

By

Kikosi cha soka akina dada humu nchini Harambee Starlets kimeondoka mapema leo kuelekea mjini Dar es Salaam Tanzania kwa mashindano ya CECAFA baina ya mataifa  Afrika ya Mashriki.

Vipusa hao chini ya kocha Beldine Odemba ilifanya mazoezi mepesi hapo jana kabila ya kukwea pipa hii leo wachezaji 23 wakisafiri ikiwa ni wachezaji wa kimataifa na wanaocheza ligi ya nyumbani.

Starlets wanafungua kampeini Jumapili dhidi ya Burundi kabila ya kumenyana na Uganda ,Sudan Kusini na badaye kumaliza na wenyeji Tanzania.

Kwa mujibu wa kocha Beldine ni kwamba amekichagua kikosi chenye ubora huku badhi ya majina makubwa yakikosekana akiwemo mshmabulizi wa Simba Queens Jentrix Shikangwa,Teresah Engesha pamoja na Mwanahalima Dogo wote wanakosekana kwenye kambi hiyo ya Starlets.

Mechi zote zinapigwa katika uwanja wa Azam Sports Complex mjini Dar es Salaam.

Continue Reading

Trending