Connect with us

Sports

Thomas Frank Kocha Mpya Spurs!

Published

on

Kilabu ya Tottenham Hotspurs kumtangaza kocha wa sasa wa Brenford Thomas Frank kuwa kocha mpya wa kilabu hiyo kumrithi Ange Postecoglou aliyepigwa kalamu wiki jana kutokana na msururu wa matokeo duni.

Kulingana na mkali wa taarifa Uhamisho barani Ulaya Fabrizio Romano ni kwamba makubaliano ya pande zote mbili zimafikiwa huku Spurs wakiwa tayari kulipia ada ya pauni milioni 10 ikiwa ni kifungu kilichomo kwenye mkataba wa kocha huyo kabila kukamilisha usajili huo.

Duru za kuaminika zaarifu kwamba mwalimu huyo amekubaliana na kilabu hiyo kwa matakwa ya binafsi na yuko tayari kuanza upya na kilabu hiyo ya London Kaskazini msimu ujao.

Raia huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 51 aliongoza Brenford kumaliza kumi bora msimu uliopita na alama 56.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Beldine Odemba Angali Kocha Wa Starlets.

Published

on

By

Mkufunzi wa Harambee Starlets Beldine Odemba atarejea kunoa tena kikosi hicho kwenye kinyanganyiro cha Cecafa ukanda wa Afrika Mashariki nchini Tanzania.

Haya yanajiri saa chache tu baada ya mwalimu huyo kubatilisha uwamuzi wake wa awali wa kujiuzulu wadhifa wake kwa kukosa ungwaji mkono kwenye majukumu yake ndaani ya vipusa hao.

Hata hivyo inaaminika baada ya kikao na Rais wa FKF Hussein Mohammed mwafaka imepatikana na sasa kocha huyo anasalia usukani kuiongoza Starlets kombe la cecafa taji ambalo linaanza mwishoni mwa jumaa.

Kocha huyo ambaye ni bingwa na kilabu ya Kenya Bullets alitangaza kujiuzulu baada ya kichapo cha magoli 5-1 mikononi mwa Morocco mechi ya kirafiki.

Continue Reading

Sports

Martin Zubimendi Kutua Arsenal

Published

on

By

Kilabu ya Arsenal imekubaliana na kiungo wa Real Sociadad Martin Zubimendi kuhusiana na uhamisho wa pauni milioni 51.

Raia huyo wa Uhispania mwenye umri wa miaka 26 sasa anatarajiwa kuwasili mjini London kwa vipimo vya kimatibabu baada ya kukubali kutua Emirates.

Haya yanajiri baada kuwepo kwa ripoti nchini Uhispania kwamba Real Madrid walikua wameingia kwenye kinyanganyiro cha kusaka huduma za kiungo huyo mbunifu.

Kulingana na mkali wa taarifa za Uhamisho barani ulaya Fabrizio Romano ni kwamba mchezaji huyo amekubali kuwasili London baada kukuabaliana na matakwa yake binafsi na yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano.

Mchezaji huyo atakua sajili wa kwanza msimu huu kwa kocha mkuu Mikel Arteta.

Continue Reading

Trending