Connect with us

News

Spika Mwambire Alalamikia Kucheleweshwa kwa Fedha za Kaunti

Published

on

 

Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi Teddy Mwambire amelalamikia hatua ya serikali kuu kuchelewesha usambazaji wa fedha za serikali za kaunti, akidai kwamba hatua hiyo imelemaza utendakazi mashinani.

Mwambire amesema hali hiyo huenda ikachangia idadi ya wafanyakazi ikiwemo maafisa wa mabunge ya kaunti sawa na viongozi wa mabunge hayo kupunguzwa.Aidha amesema licha ya changamoto hiyo, wafanyakazi wa bunge la kaunti ya Kilifi wamekuwa wakitekeleza majukumu yao kwa bidii kwa lengo la kuboresha gatuzi la Kilifi.

Wakati huo huo amesifia bunge la kaunti ya Kilifi akilitaja kama bunge bora zaidi kwani halijahusishwa na matumizi mabaya ya fedha za umma jinsi inavyoshuhudiwa katika mabunge mengine ya kaunti humu nchini.

Kiongozi huyo hata hivyo amesema hali hiyo inadhihirisha wazi kwamba viongozi ndani ya bunge hilo wanalenga zaidi matakwa ya wananchi na wala sio kujinufaisha binafsi.

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Chama cha DCP chashinikiza wakenya kupinga mswada wa fedha wa mwaka 2025/26.

Published

on

By

Uongozi wa chama cha DCP chake Rigathi Gachagua sasa unashinikiza wakenya kupinga mswada wa fedha wa mwaka 2025/26 ukidai unavipengee tata vitakavyoongeza mzigo wa ushuru kwa wakenya.

Kulingana na naibu kinara wa chama hicho Cleophas Malala mswada huo hauzingatii hali ya uchumi kwa wakenya ambao wanaendelea kukabiliana na gharama ya juu ya maisha.

Malala alitaja baadhi ya vipee vinavyoibua maswali kama vile kodi mpya ya kuongezwa kwa ushuhru wa VAT kwenye bidhaa za kawaida kama vile vyakula.

Akizungumza mjini Mombasa Malala alishauri wakenya kuwa makini na kushiriki mchakato wa kuchambua mswada huo kikamilifu vile vile kutoa maoni kwa bunge kabla ya kupitishwa na kuwa sheria.

Vile vile Malala alimlaumu kinara wa chama cha ODM Raila Odinga pamoja na Rais William Ruto akidai wamehadaa familia zilizowapoteza wapendwa wao mwaka jana wakati wa kupinga mswada wa fedha kwamba zingefidiwa.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Mamlaka ya KPA yalalamikia changamoto zinazolemaza shughuli zake.

Published

on

By

Licha ya Bandari ya Mombasa kuendelea kurekodi matokeo bora katika utendakazi wake,mamlaka ya bandari nchini (KPA) imebainisha kwamba bado kuna changamoto zinazolemaza shughuli zake.

Akizungumza katika kikao na kamati ya bunge kuhusu ushirikiano wa kikanda, mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya KPA, Nahodha William Ruto, alieleza kuwa changamoto hizo ni pamoja na idadi kubwa ya mashirika yanayokagua mizigo, vizuizi vya kupima uzito wa magari (weighbridges), na vizuizi vya polisi barabarani katika eneo la Kaskazini (Northern Corridor).

Kulingana na nahodha Ruto hali hiyo bado inaathiri ufanisi wa usafirishaji wa mizigo na biashara kwa ujumla.

Nahodha Ruto pia alieleza athari za ada zisizo rasmi zinazotozwa na mashirika mbalimbali, pamoja na ushuru wa CESS unaotozwa na serikali za kaunti kwa mizigo ambayo tayari imekaguliwa na kulipiwa bandarini.

Aliongeza kuwa gharama hizo za ziada zinaathiri ushindani wa Kenya kama kitovu cha biashara katika ukanda wa afrika mashariki.

Wakati uo huo, Ruto aliitaka serikali kuharakisha uboreshaji wa mifumo ya usafirishaji kwa kuongeza matumizi ya teknolojia na kuunganisha mifumo ya upimaji wa uzito wa magari kote nchini.

Kwa upande wake, kamati ya bunge kupitia kwa mwenyekiti wake, Bi. Irene Mayaka, iliahidi kwamba kamati hiyo itafuatilia kwa karibu malalamshi yaliyoibuliwa na kuhakikisha kwamba suluhu mwafaka inapatikana.

Taarifa ya mwanahabari wetu.

Continue Reading

Trending