News
Spika Mwambire Alalamikia Kucheleweshwa kwa Fedha za Kaunti

Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi Teddy Mwambire amelalamikia hatua ya serikali kuu kuchelewesha usambazaji wa fedha za serikali za kaunti, akidai kwamba hatua hiyo imelemaza utendakazi mashinani.
Mwambire amesema hali hiyo huenda ikachangia idadi ya wafanyakazi ikiwemo maafisa wa mabunge ya kaunti sawa na viongozi wa mabunge hayo kupunguzwa.Aidha amesema licha ya changamoto hiyo, wafanyakazi wa bunge la kaunti ya Kilifi wamekuwa wakitekeleza majukumu yao kwa bidii kwa lengo la kuboresha gatuzi la Kilifi.
Wakati huo huo amesifia bunge la kaunti ya Kilifi akilitaja kama bunge bora zaidi kwani halijahusishwa na matumizi mabaya ya fedha za umma jinsi inavyoshuhudiwa katika mabunge mengine ya kaunti humu nchini.
Kiongozi huyo hata hivyo amesema hali hiyo inadhihirisha wazi kwamba viongozi ndani ya bunge hilo wanalenga zaidi matakwa ya wananchi na wala sio kujinufaisha binafsi.
News
Macharia: Jamii ya Kilifi kusini watapeliwa ardhi kufuatia ukosefu wa Elimu

Msaidizi wa Kamishna wa kaunti ya Kilifi eneo la Kilifi Kusini, Francis Macharia amesema ukosefu wa elimu umechangia kwa wanajamii wengi kaunti ya Kilifi kutapeliwa katika umiliki wa ardhi.
Akizungumza eneo la Vipingo, Macharia alisema kuwa wanajamii wengi hasa wazee wamekuwa wakitapeliwa mashamba yao kutokana na kukosa kisomo.
Macharia alisisitiza haja ya jamii kuzingatia elimu kwani visa vya ulaghai wa mashamba kutokana na ukosefu wa elimu vimekithiri mno hasa mashanani.
“Kuna baadhi ya vijana pia wamekuwa wakiwatapeli wazazi wao fedha za inua jamii pindi zinapotumwa, na hii imechangiwa na kutosoma wazee hao” aliongeza Macharia.
Macharia alisema wazazi pia wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa wanao wanapata elimu ipasavyo akisema kuwa eneo la Kilifi kusini limekuwa na visa vingi vya watoto wanaoacha shule na kuingilia vibarua.
Taarifa ya Hamis Kombe
News
Makalo atoa wito kwa serikali kuendeleza mpango wa ugavi wa chakula

Mwakilishi wa wadi ya Kasighau kaunti ya Taita Taveta Amos Makalo ametoa wito kwa serikali kuu kuendeleza mpango wa ugavi wa chakula cha msaada katika eneo hilo sawa na maeneo mengine kote nchini ili kunusuru maelfu ya wananchi wanaokabiliwa na baa la nja.
Makalo alisema chakula hicho ni kidogo mno kwani wananchi wengi wa Kasighau pamoja na maeneo mengine ya kaunti hiyo wanakabiliwa na baa la njaa.
Wakati huohuo Makalo alimshinikiza mwakilishi wa kike kwenye kaunti hiyo Lydia Haika kuishawishi serikali kuu kuikumbuka kaunti hiyo katika kupeana misaada mbalimbali ambayo itawafaidi wenyeji.
“Wananchi wanahangaika kutokana na njaa. Na kwasababu umetutembelea na mazuri leo wacha niombe kwamba hayo Mazuri yaendelee kwa muda huu ulio mbele yetu maana hali ni ngumu sana’’
Haya yanajiri huku Serikali ya kitaifa kupitia wizara ya huduma za kitaifa na mipango maalum ikiendeleza shughuli za usambazaji wa chakula cha msaada kwa wahanga wa baa la njaa kaunti ya Taita Taveta na maeneo mengine nchini.
Taarifa ya Janet Mumbi
-
Sports10 hours ago
Harambee Stars Wapiga Ushelisheli Kasarani, Olunga Asawazisha Rekodi ya Oliech
-
News9 hours ago
Viongozi wa jamii ya Mijikenda wakosoa maandazili ya sherehe za Chenda chenda.
-
Sports6 hours ago
Uingereza yawapa wapinzani onyo baada ya kuichapa Serbia 5-0, Haaland apiga mabao matano kwa Norway