Connect with us

News

Spika Mwambire Alalamikia Kucheleweshwa kwa Fedha za Kaunti

Published

on

 

Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi Teddy Mwambire amelalamikia hatua ya serikali kuu kuchelewesha usambazaji wa fedha za serikali za kaunti, akidai kwamba hatua hiyo imelemaza utendakazi mashinani.

Mwambire amesema hali hiyo huenda ikachangia idadi ya wafanyakazi ikiwemo maafisa wa mabunge ya kaunti sawa na viongozi wa mabunge hayo kupunguzwa.Aidha amesema licha ya changamoto hiyo, wafanyakazi wa bunge la kaunti ya Kilifi wamekuwa wakitekeleza majukumu yao kwa bidii kwa lengo la kuboresha gatuzi la Kilifi.

Wakati huo huo amesifia bunge la kaunti ya Kilifi akilitaja kama bunge bora zaidi kwani halijahusishwa na matumizi mabaya ya fedha za umma jinsi inavyoshuhudiwa katika mabunge mengine ya kaunti humu nchini.

Kiongozi huyo hata hivyo amesema hali hiyo inadhihirisha wazi kwamba viongozi ndani ya bunge hilo wanalenga zaidi matakwa ya wananchi na wala sio kujinufaisha binafsi.

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.

Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.

Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.

Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Published

on

By

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.

Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.

Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.

Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.

Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending