Sports
Sinner Bingwa Tennis Msururu Wa Wimbledon

Mchezaji wa Tenisi anayeorodheshwa wa kwanza Ulimwenguni Jennik Sinner raia wa Italia amesema kwamba lengo lake ni kutawala dunia sasa baada ya kumpiku mwenzake Carlos Alcaraz na ksuhinda fainali ya taji la Wimbledon likiwa ni taji lake la kwanza.
Sinner alimpiku Alcaraz raia wa Uhispania kwa seti za 4-6, 6-4, 6-4, 6-4 na kuvunjilia mbali rekodi ya mhispania huyo ya kushinda taji hilo mara tatu mfululizo.
Mchezaji huyo amesema kwamba analenga kujiboresha hata zaidi akiwaonya wapinzani angali kutoa makali yake yote.
“Niko na umri wa miaka 23 na kwa sasa ningali kuwa katika ubora wangu narudi kujipanga zaidi kwa ajili ya misururu mingine ila niko na imani ya kufanya kweli katika misuru ya Tenisi.”
Mchezaji huyo amfika katika fainali nne na kushinda tatu za Grandslam na amesema hataki kutoka hapo juu kuwa mchezaji bora.
Sports
Harambee Stars Kundi La Kifo Kundi B.

Sports
Kiungo Wa Brenford Bryan Mbeumo Sasa Ni Mali Ya United

Baada ya vute ni kuvute ambayo imedumu kwa kipindi cha mwezi mmoja ni rasmi kwamba kilabu ya manchester United na Brenford wameafikia makubaliano ya pauni milioni 70 ya kiungo mshambulizi Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.
Haya yanajiri baada ya ofa mara mbili ya united kukataliwa na kilabu hio kabila ya kutuma ofa ya mwisho ya pauni milioni 65 na nyongesa ya pauni milioni 5.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano baada kukubali matakwa yake binafsi.
Mbeumo anakua sajili wa pili kwa kocha mkuu Ruben Amorim baada ya ujio wa mshmabulizi Matheus Cunha.