Sports
Sinner Bingwa Tennis Msururu Wa Wimbledon

Mchezaji wa Tenisi anayeorodheshwa wa kwanza Ulimwenguni Jennik Sinner raia wa Italia amesema kwamba lengo lake ni kutawala dunia sasa baada ya kumpiku mwenzake Carlos Alcaraz na ksuhinda fainali ya taji la Wimbledon likiwa ni taji lake la kwanza.
Sinner alimpiku Alcaraz raia wa Uhispania kwa seti za 4-6, 6-4, 6-4, 6-4 na kuvunjilia mbali rekodi ya mhispania huyo ya kushinda taji hilo mara tatu mfululizo.
Mchezaji huyo amesema kwamba analenga kujiboresha hata zaidi akiwaonya wapinzani angali kutoa makali yake yote.
“Niko na umri wa miaka 23 na kwa sasa ningali kuwa katika ubora wangu narudi kujipanga zaidi kwa ajili ya misururu mingine ila niko na imani ya kufanya kweli katika misuru ya Tenisi.”
Mchezaji huyo amfika katika fainali nne na kushinda tatu za Grandslam na amesema hataki kutoka hapo juu kuwa mchezaji bora.
Sports
Makocha Saba pekee Wameshinda Taji La CHAN

CHAN COUNT DOWN 16 Days to Go
Sports
Matumaini Ya United Kupata Mbeumo Yanazidi Kudidimia

Matumaini ya kilabu ya manchester united kupata huduma za kiungo mshambulizi wa kilabu ya Brenford Bryan Mbeumo yanaonekana kufifia kila kuchao.
Haya yanajiri baada ya mazungumzo hayo kukwama kwa sasa baada ya kilabu hiyo ya London kuongeza ada ya malipo ya mchezaji huyo hadi pauni milioni 70.
Kilabu ya Manchester United haiko tayari kulipa zaidi ya pauni milioni 65 kwa mvamizi huyo raia wa Cameroon.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alifunga magoli 20 ligi ya epl msimu jana.