News
Shule Ya Upili Ya Serani Ndiyo Mabingwa Eneo La Mvita

Timu ya shule ya upili ya Serani imetetea ubingwa wao wa eneo la Mvita baada ya kuwalaza Tononoka magoli 2-1 katika fainali iliyochezewa kwenye uwanja wa shule ya upili ya Khamis.
Emanuel Oroni aliwatanguliza Serani na goli la kwanza kupitia mkwaju wa penati kabla ya Ali Abdallah kusawazishia Tononoka, lakini goli lake Emanuel Ngala katika kipindi cha pili likawapa ubingwa huo.
Kulingana na kocha wa Serani Alex Shikanga ni kwamba wamekua na mazoezi kambambe kabila ya mashindano ya shule za Upili na walikua wanasubiri ushindi tu wala si kitu kingine.
“Tulikua tumejiandaa kwa ajili ya ushindi pekee tumekua na maandalizi mazuri na hivyo nilijua tuatshinda fainali hii,katika miaka mitano tumepoteza taji hili mara moja pekee.”
kwa upande wake kocha wa Shule ya Upili ya Tononoka Juma ALi Kalato amesema kwamba amesema kwamba amekubali matokeo baada ya changamoto si haba kabila ya mechi hiyo ya fainali baadhi ya wachezaji wakingonjeka.
“Nashukuru Mwenyemezi Mungu tumefika fainali na vijana wangu wamepambana kiume kwani kabila ya mechi tulikua na wagonjwa ila wamepambana inshallah tutashinda uko mbele.”
Katika upande wa wasichana Kaa Chonjo wameibuka mabingwa kwa kuwalaza Mekatitilili magoli 3-0.
Serani na Tononoka wataiwakilisha Mvita katika ngazi ya kaunti upande wa wavulana, na Kaa Chonjo na Mekatililii wakiwakilishja upande wa wasichana.
News
Wahudumu wa afya Lamu watishia kuishtaki serikali ya kaunti hiyo

Wahudumu wa Afya kaunti ya Lamu wametishia kuelekea Mahakamani kuishtaki serikali ya kaunti hiyo kwa kukaidi kutekeleza matakwa yao.
Wahudumu hao waliishtumu serikali ya kaunti ya Lamu kwa kupuuza matakwa yao na badala yake kutumia vitisho ili kuwashurutisha kurejea kazini.
Kulingana na viongozi wa wahudumu hao, licha ya mgomo wao kuendelea kwa zaidi ya wiki mbili serikali ya kaunti hiyo imekataa kata kuandaa vikao vya kusuluhisha malalamishi yao.
Baadhi ya changamoto wanazolalamikia ni pamoja na kufanya kazi kwa zaidi ya miaka 10 bila ya kupandishwa vyeo, kupuuzwa kwa mkataba wa makubaliano ya nyongeza ya mishahara, kunyimwa kwa mishahara kwa baadhi ya wahudumu hao miongoni mwa matakwa mengine.
“Mkiendelea kutufinyilia itabidi tufuate njia ya sheria kwa sababu tunajua tunalilia haki yetu, haiwezekani serikali ya kaunti inashindwa kutupandisha vyeo ilhali tumefanya kazi kwa miaka 15 sasa, hatuwezi kuendelea kufanya kazi katika mazingira duni na pia mkataba wa makubaliano kuhusu nyongeza ya mishahara sharti itekelezwe” walisisitiza viongozi hao.
Wakati uo huo serikali ya kaunti ya Lamu imejibu malimishi yao kupitia barua na kutangaza kuwa mgomu huo ni kinyume cha seria na kuwataka wahudumu hao kurejea kazini mara moja.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Rais Ruto atuma KDF kusimamia ujenzi wa hospitali nchini

Rais William Ruto ametuma jeshi la KDF kusimamia ujenzi wa vituo vya afya zaidi ya 75 kote nchini katika juhudi za kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa haraka.
Akizungumza katika kaunti ya Narok wakati wa uzinduzi wa hospitali ya Sogoo Level 4, waziri wa ulinzi Patrick Mariru alifichua kuwa ujenzi wa hospitali hiyo yenye mamlaka kamili itakamilika baada ya mda wa miezi 11.
Ujenzi wa hospitali ya Sogoo Level 4 ulivutia rais Ruto alipozuru eneo hilo mwezi mei mwaka 2025, jambo lililomfanya kuagiza KDF kuipandisha hadhi.
Mariru hata hivyo alishikilia kuwa wafanyikazi wote wasio na ujuzi watatolewa kutoka kwa jamii.
“Jeshi litamsimamia mkandarasi. Hilo liwe wazi, kazi yote itafanywa na vijana wa Sogoo. Tutaweka maafisa wawili na kila jioni watanipa ripoti ya maendeleo,” alisema Mariru.
“Tuna zaidi ya miradi 75 tunayosimamia na sio kwamba tunabadilisha wakala wa serikali tunataka tu kushirikiana na ofisi tofauti miongoni mwao wizara za afya na michezo.”
Taarifa ya Joseph Jira