Connect with us

News

Serikali yatoa shilingi milioni 60 kwa waathiriwa wa mafuriko Tana River

Published

on

Serikali ya kitaifa imezindua mpango wa msaada wa shilingi milioni 60 kwa wakazi wa Tana River walioathiriwa na mafuriko ya kudumu.

Mpango huo ulizinduliwa na katibu mkuu wa mipango maalum Ismail Maalim na mwenzake wa maswala ya kuangazia ardhi kame- ASALS Kello Harsama siku ya jumatatu 16, juni 2025.

Akizungumza katika eneo la Majengo, Maalim alisisitiza umuhimu wa zoezi hilo akisema ni wajibu wa kikatiba kwa serikali kutoa msaada wa chakula kwa wananchi wake.

Maalim aliongeza kuwa zaidi ya wakenya milioni 2 watapokea msaada wa chakula kutoka kwa serikali.

Kwa upande wake, Harsama alisema serikali tayari imesambaza mabati kwa waathiriwa wa mafuriko katika kaunti hiyo wakiwemo watu 600 walioathirika na mafuriko katika eneo bunge la Galole.

Makatibu hao walizuru kaunti nzima wakisambaza chakula cha msaada, magodoro na blanketi kwa wakazi, wakiandama na mbunge wa Garsen Ali Wario, mbunge wa Galole Said Buya na Mbunge wa Bura Yakub Adow.

Taarifa na Joseph Jira.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Published

on

By

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.

Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.

“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi

Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.

Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending