Connect with us

News

Serikali yatenga shilingi milioni 250 kwa Walemavu.

Published

on

Serikali kupitia Wizara ya Leba na maslahi ya kijamii imetenga shilingi milioni 250 mwaka wa 2025 ili kuimarisha uwezeshaji wa watu wanaoishi na ulemavu nchini.

Katibu mkuu wa wizara hiyo Joseph Motari alitangaza kuwa ufadhili huo utasaidia masuala ya elimu, kuwawesha kiuchumi pamoja na teknolojia kwa jamii hiyo.

Motari alibainisha hayo wakati wa kikao cha 18 cha mkutano wa nchi wanachama wa mkataba wa haki za watu wenye ulemavu (CRPD) jijini New York nchini Marekani.

“Kenya inaongeza juhudi zake za kujumuisha uchumi kwa kutenga zaidi ya shilingi milioni 250 mwaka huu kupitia msaada wa elimu, uwezeshaji wa kiuchumi na msaada wa kiteknolojia”, Motari alisema.

Katibu huyo pia aliangazia utekelezaji wa mpangilio wa mkakati wa mwaka 2023-27 ambao unayapa kipaumbela masuala ya ufahamu, uwezeshaji wa kijamii na kiuchumi, vile vile ujumuishaji wa kidijitali kwa watu wanaoishi na ulemavu.

Kulingana na Motari, takribani makaazi elfu 63 yatanufaika na program za serikali za kusambaza pesa na upokezaji wa marupurupu ya kila mwezi ya shilingi elfu mbili.

Kati ya hao zaidi ya walengwa elfu 20 wanafadhiliwa chini ya mpango ujulikanao kama Autism and Developmental Disabilities programme.

Mwaka 2024, serikali ilisambaza takriban vifaa 4,200 vya usaidizi kwa jamii hiyo pamoja na kutoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi 2,500 wanaoishi na ulemavu.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Nassir: Kaunti ya Mombasa wametenga milioni 80 za Afya

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Mombasa, Abdulswamad Shariff Nassir amesema serikali ya kaunti ya Mombasa wametenga shilingi milioni 80 kugharamia sehemu ya matibabu ya wakaazi ambao hutibiwa katika hospitali za Level 4 na Level 5.

Akizungumza katika kaunti ya Mombasa, Nassir alisema fedha hizo zitagharamia bima ya afya ya SHA ya wenyeji wa kaunti hiyo kwa muda wa mwaka mmoja.

Gavana Nassir pia alisema fedha hizo zitagharamia madeni ya ziada ya matibabu kwa watoto wa chini ya umri wa miaka 5 ambao wanatibiwa kupitia bima hiyo ya SHA.

“Tumeweka dawati maalum na fedha kuweza kuwalipia ile amana ambayo ilikuwa inalipiwa SHA. Na itakuwa sio ya Public health pekee lakini kando na Public health mnakuwa mumelipiwa kwa mwaka mzima’’, alisema gavana Nassir

Wakati huo huo Gavana Nassir alieleza matumaini kwamba mpango huo utasaidia kwa asilimia kubwa kuimarisha huduma za matibabu kwa wenyeji wa kaunti hiyo.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Chibule, apendekeza adhabu kali kwa wanaoendeleza dhulma za kijinsia

Published

on

By

Naibu gavana kaunti ya Kilifi Flora Mbetsa Chibule, amependekeza adhabu kali kwa watu wanaotekeleza visa vya dhulma za kijinsia katika jamii.

Chibule alisema visa vya dhulma za kijinsi dhidi ya watoto vimekithiri katika jamii hasa kaunti ya Kilifi, akiahidi ushirikiano wa hali ya juu na wadau mbalimbali ili kukomesha visa hivyo.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya hamasa kuhusu dhulma za kijinsia katika uwanja wa Bofa Youth mjini Kilifi, Chibule alisema ili kufanikisha ndoto ya mtoto wa kike ni lazima haki zao za kimsingi zilindwe.

“Kwa ambao wanadhulumu mtoto wa kike na kiume, kwa wale ambao wanaingia misuli kwa misuli wanafaa kuwekwa gerezani kabisa”, alisema Chibule.

Wanaharakati wa kijamii wapinga unyanyasaji wa kijinsi, Kilifi

Kwa upande wake Mwakilishi wa kike kaunti ya Kilifi Getrude Mbeyu aliyeandaa hafla hiyo kupitia hazina ya kitaifa ya NGAAF na kutoa hundi ya kima cha shilingi milioni 1.6 kwa makundi 14, alisisitiza hamasa zaidi kwa jamii kuhusu jinsi ya kukomesha visa hivyo.

“Ni jukumu letu la kuwaeleza hawa watu watambua jinsi ya kuripoti hizi kesi, yani kwa mfano umedhulumiwa ni wapi pa kuanzia na hatua hii itakomesha hizi visa”, alisema Mbeyu.

Naye Mzee wa mataa wa Kiwandani mjini Kilifi Elina Nyevu alisema visa vya dhulma za kimapenzi vimekithiri mno katika mtaa huo, akipendekeza hamasa zaidi kwa jamii.

“Hapa kwetu Kiwandani visa vya dhulma za kijinsia ni vingi sana, kuna ulevi na ukosefu wa ajira ambao umechangia utumiaji wa Mihadarati na unyanyasaji wa watoto wadogo kimapenzi, alisema Elina.

Hata hivyo katika halfa hiyo baadhi ya watoto waliopitia madhila hayo hasa ubakaji wameelezea masaibu waliopitia japo haki yao kupitia idara ya usalama walikosa kufaulu.

Taarifa ya Lolani Kalu.

Continue Reading

Trending