Connect with us

News

Serikali yatenga shilingi milioni 250 kwa Walemavu.

Published

on

Serikali kupitia Wizara ya Leba na maslahi ya kijamii imetenga shilingi milioni 250 mwaka wa 2025 ili kuimarisha uwezeshaji wa watu wanaoishi na ulemavu nchini.

Katibu mkuu wa wizara hiyo Joseph Motari alitangaza kuwa ufadhili huo utasaidia masuala ya elimu, kuwawesha kiuchumi pamoja na teknolojia kwa jamii hiyo.

Motari alibainisha hayo wakati wa kikao cha 18 cha mkutano wa nchi wanachama wa mkataba wa haki za watu wenye ulemavu (CRPD) jijini New York nchini Marekani.

“Kenya inaongeza juhudi zake za kujumuisha uchumi kwa kutenga zaidi ya shilingi milioni 250 mwaka huu kupitia msaada wa elimu, uwezeshaji wa kiuchumi na msaada wa kiteknolojia”, Motari alisema.

Katibu huyo pia aliangazia utekelezaji wa mpangilio wa mkakati wa mwaka 2023-27 ambao unayapa kipaumbela masuala ya ufahamu, uwezeshaji wa kijamii na kiuchumi, vile vile ujumuishaji wa kidijitali kwa watu wanaoishi na ulemavu.

Kulingana na Motari, takribani makaazi elfu 63 yatanufaika na program za serikali za kusambaza pesa na upokezaji wa marupurupu ya kila mwezi ya shilingi elfu mbili.

Kati ya hao zaidi ya walengwa elfu 20 wanafadhiliwa chini ya mpango ujulikanao kama Autism and Developmental Disabilities programme.

Mwaka 2024, serikali ilisambaza takriban vifaa 4,200 vya usaidizi kwa jamii hiyo pamoja na kutoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi 2,500 wanaoishi na ulemavu.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Published

on

By

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.

Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.

“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi

Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.

Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending