Connect with us

News

Serikali yafidia wakaazi wa mzozo wa Wanyamapori milioni 60

Published

on

Serikali ya kitaifa kupitia Wizara ya Utalii na wanyamapori nchini imetoa kima cha shilingi milioni 60 za fidia kwa wakaazi walioathirika na mizozo ya wanyamapori katika kaunti ya Kilifi.

Akizungumza wakati wa hafla ya kutoa fedha hizo katika wadi ya Marafa eneo bunge la Magarini, Waziri wa Utalii nchini Rebecca Miano alisema fedha hizo zitafidia visa zaidi ya 1,300 vya watu walioathirika na mizozo hiyo tangu mwaka 2021 kaunti ya Kilifi.

Miano alikariri kwamba mizozo ya Wanyamapori kaunti ya Kilifi imeathiri sana maeneo ya Magarini, Ganze na Vitengeni na kuchangia uharibifu wa mimea na hata maafa, akidai kwamba serikali imeweka mikakati kabambe ya kukomesha mizozo hiyo.

Kwa upande wake Naibu gavana wa Kilifi Flora Chibule alielezea matumaini ya kupatikana kwa suluhu la kudumu kwa mizozo hiyo hasa kutokana na mikakati iliyowekwa na serikali ili kutatua suala hilo.

Viongozi na wakaazi katika mkutano wa fidia ya wanyamapori

Wakati huo huo serikali imefichua kuwa imeweka kikosi maalum cha dharura cha maafisa wanaoshughulikia visa vya uvamizi wa wanyamapori kaunti ya Kilifi ikilenga kukabiliana na visa hivyo ili kulinda maisha ya wakaazi.

Haya yanajiri huku tayari serikali ya kitaifa ikiwa imetoa jumla ya shilingi bilioni 2.8 kote nchini za fidia kwa wananchi walioathiriwa na wanyamapori katika awamu ya kwanza huku shilingi bilioni 1.36 zikitarajiwa kutolewa siku zijazo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Published

on

By

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.

Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.

Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.

“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

News

Mahakama ya Kilifi yaanzisha upya kesi ya ulaghai wa pesa

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imeanzisha upya kesi ya mwanaume mmoja anayekabiliwa na shtaka la ulaghai wa pesa.

Hii ni baada ya Mwanaume huyo kwa jina Samuel Ngonyo, kuachiliwa kwa dhamana hapo awali lakini alikosa kudhuhuria vikao Mahakamani hali iliyopelekea kesi hiyo kuanzishwa upya.

Hakimu mkuu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa aliagiza jamaa huyo kuzuliwa rumande baada ya agizo la kukamatwa kwake kuidhinishwa na Mahakama baada ya jamaa huyo kupuuza vikao vya Mahakama vya awali.

Kabla ya agizo hilo, Mahakama ilielezwa kwamba mnamo tarehe tofauti kati ya mwezi Septemba hadi Oktoba mwaka 2021 katika maeneo la Ganze kaunti ya Kilifi kwa kutumia njia ya ulaghai, mshukiwa alichukua pesa taslimu shilingi elfu 50 ya mlalamishi Grace Sidi Katana.

Mahakama ilielezwa zaidi kwamba mshukiwa alitekeleza kitendo hicho baada kumdanganya Mlalamishi kwamba yeye ni Mwandishi na afisa wa kazi za umma hivyo angemsaidia Moses Katana mtoto wa mlalamishi kupata kazi ya serikali.

Kesi hiyo itaendelea mnamo tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending