Connect with us

News

Serikali yafidia wakaazi wa mzozo wa Wanyamapori milioni 60

Published

on

Serikali ya kitaifa kupitia Wizara ya Utalii na wanyamapori nchini imetoa kima cha shilingi milioni 60 za fidia kwa wakaazi walioathirika na mizozo ya wanyamapori katika kaunti ya Kilifi.

Akizungumza wakati wa hafla ya kutoa fedha hizo katika wadi ya Marafa eneo bunge la Magarini, Waziri wa Utalii nchini Rebecca Miano alisema fedha hizo zitafidia visa zaidi ya 1,300 vya watu walioathirika na mizozo hiyo tangu mwaka 2021 kaunti ya Kilifi.

Miano alikariri kwamba mizozo ya Wanyamapori kaunti ya Kilifi imeathiri sana maeneo ya Magarini, Ganze na Vitengeni na kuchangia uharibifu wa mimea na hata maafa, akidai kwamba serikali imeweka mikakati kabambe ya kukomesha mizozo hiyo.

Kwa upande wake Naibu gavana wa Kilifi Flora Chibule alielezea matumaini ya kupatikana kwa suluhu la kudumu kwa mizozo hiyo hasa kutokana na mikakati iliyowekwa na serikali ili kutatua suala hilo.

Viongozi na wakaazi katika mkutano wa fidia ya wanyamapori

Wakati huo huo serikali imefichua kuwa imeweka kikosi maalum cha dharura cha maafisa wanaoshughulikia visa vya uvamizi wa wanyamapori kaunti ya Kilifi ikilenga kukabiliana na visa hivyo ili kulinda maisha ya wakaazi.

Haya yanajiri huku tayari serikali ya kitaifa ikiwa imetoa jumla ya shilingi bilioni 2.8 kote nchini za fidia kwa wananchi walioathiriwa na wanyamapori katika awamu ya kwanza huku shilingi bilioni 1.36 zikitarajiwa kutolewa siku zijazo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending