Connect with us

News

Seneta Cherargei, Anataka Waziri Murkomen Kujiuzulu

Published

on

Baadhi ya viongozi wa kisiasa wamemtaka Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen kujiuzulu kwa madai kwamba ameshindwa kuimarisha usalama katika maeneo mbalimbali ya taifa.

Wakiongozwa na Seneta wa Nandi Samson Cherargei, Viongozi hao wamesema Waziri Murkomen umeonyesha wazi kutowajibika katika majukumu yake pamoja na kushindwa kupanga kikamilifu usalama wa taifa.

Cherargei amemtaka rais William Ruto kumhamisha Waziri Murkomen katika Wizara hiyo na kumpa wadhfa wa ubalozi katika mataifa ya Pakistan, Gaza ama nchini Tanzania ili kushughulikia masuala ya kidiplomasia.

Cherargei anasema masuala ya usalama huwezi kufananisha na masuala ya barabara kwani usalama wa wananchi ni muhimu zaidi na kutowajibika kwa Waziri Murkomen kumechangia wakaazi wa maeneo ya Kerio Valley kupoteza maisha yao.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.

Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.

Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.

Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Published

on

By

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.

Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.

Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.

Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.

Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending