Sports
Real Madrid Kuanza Rasmi msimu Mpya wa Laliga Chini Ya Xabi Alonso

Kocha wa Real Madrid, Xabi Alonso, amesema maandalizi mafupi ya kabla ya msimu hayatakuwa kisingizio huku kikosi chake kikijiandaa kuanza kampeni ya La Liga nyumbani dhidi ya Osasuna leo usiku.
Mchezaji huyo wa zamani wa Real atakuwa akisimamia mchezo wake wa kwanza katika uwanja wa Santiago Bernabeu baada ya kuanza rasmi enzi yake kwenye Kombe la Dunia la Klabu nchini Marekani, ambapo Madrid walitinga hatua ya nusu fainali.
Awali ombi la Madrid la kuahirisha mechi yao ya ufunguzi wa ligi hadi tarehe nyingine lilikataliwa na viongozi wa soka la Uhispania, na kikosi hicho kimecheza mechi moja tu ya kirafiki tangu waliposhindwa 4-0 dhidi ya Paris Saint-Germain huko New Jersey mnamo Julai 9.
Alonso sasa anategemea usajili kadhaa wapya, akiwemo beki wa zamani wa Liverpool Trent Alexander-Arnold, wakati Madrid wakilenga kufuta kumbukumbu ya mwisho mbaya wa enzi ya Carlo Ancelotti.
Madrid walitwaa Kombe la Klabu Bingwa Ulaya na La Liga msimu wa 2023-24, lakini wakamaliza ligi ya ndani wakiwa wa pili nyuma ya mahasimu wao wakubwa Barcelona msimu uliopita, na wakaondolewa na Arsenal katika robo fainali ya Ulaya.
Alonso, ambaye aliiongoza Bayer Leverkusen kutwaa ubingwa wa Bundesliga na Kombe la Ujerumani miaka miwili iliyopita, amesema kwa tahadhari kuhusu matarajio yake jijini Madrid.
Sports
Shirika la Kupiga Vita Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) Lawashtaki Kenya kwa Kukosa Kutii Kanuni

Shirika la Kupambana na Matumizi ya Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) siku ya Alhamisi limeshtaki Kenya kwa kutotii masharti yake, hatua inayoweza kusababisha nchi hiyo ya Afrika Mashariki kuwekewa vikwazo mwezi ujao.
WADA, lenye makao yake Montreal, Canada, limesema kuwa shirika la kitaifa la kudhibiti matumizi ya dawa za kusisimua misuli nchini Kenya bado halijashughulikia mahitaji muhimu yaliyoainishwa baada ya ukaguzi uliofanywa mwezi Mei 2024.
Kwa sasa, Kenya ina siku 21 za kupinga madai hayo au kufanya marekebisho yanayohitajika na WADA, la sivyo itatangazwa rasmi kuwa imekosa kutii kanuni.
Kwa sasa, kuna wadau wanne waliotia saini kanuni za WADA walioko kwenye orodha ya kutotii masharti. Hawa ni pamoja na:
-
Urusi
-
Sri Lanka
-
Shirikisho la Kimataifa la Basque Pelota
-
Shirikisho la Kimataifa la Mazoezi ya Mwili na Ujenzi wa Misuli (IFBB)
Sports
Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya Ronald Bukusi Afafanua Hali ya Ukocha katika Timu ya Taifa

Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya, Ronald Bukusi, ameondoa uvumi kuhusu mpangilio wa uongozi ndani ya timu ya taifa ya kriketi ya wanaume, akisisitiza kuwa hakuna mkanganyiko wowote kuhusu majukumu ya makocha Joseph Angara na Lameck Onyango.
Akizungumza katika makao makuu ya shirikisho hilo Ruaraka, Nairobi, Bukusi alieleza kuwa benchi la kiufundi linafanya kazi kwa mshikamano, huku wachezaji hao wa zamani wa kimataifa wakikamilishana katika uwezo wao.
“Tuna makocha wawili. Inategemea tu wanachofanya siku hiyo maalum,” alisema Bukusi.
Kwa sasa, Angara ndiye kocha mkuu, huku Onyango akiwa msaidizi wake. Wawili hao walichukua majukumu hayo kwa muda tangu Septemba 2024 baada ya bodi kufuta uteuzi wa mchezaji wa zamani wa India, Dodda Ganesh, kwa sababu za ukiukaji wa taratibu.
Kwa kuzingatia kuwa mashindano ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la ICC la 2027 yanakaribia, Bukusi alisisitiza kuwa timu ya taifa imedhamiria kazi iliyo mbele yao. Mashindano hayo makubwa duniani yataandaliwa kwa pamoja na Afrika Kusini, Zimbabwe na Namibia.
“Kwa sasa, malengo yetu ni kujaribu kufika Zimbabwe na kufuzu Kombe la Dunia,” alisema Bukusi. “Tuna benchi bora la kiufundi linaloongozwa na Bw. Tariq [mwanabodi], na kwa pamoja tunashughulikia changamoto zinazoikumba timu.”
Hata hivyo, alionya kuwa mafanikio yanahitaji zaidi ya kipaji cha uwanjani, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji na utiifu wa kanuni katika mifumo yote.
“Lazima tuwe watiifu kuhusu fedha na kupiga vita matumizi ya dawa za kusisimua misuli. Sio kitu cha kufanikisha mara moja—itakuwa mchakato,” aliongeza.
Kenya itaendeleza kampeni ya kufuzu kwa kuikabili Namibia Septemba 26 katika Harare Sports Club, kisha kucheza dhidi ya Malawi Septemba 28 katika Takashinga Cricket Club. Mechi yao ya mwisho ya makundi itakuwa dhidi ya Nigeria Septemba 30.
Kenya inatarajia kurudia historia ya mwaka 2003, walipofika nusu fainali, mafanikio makubwa zaidi kuwahi kupatikana na taifa lisilocheza mechi za Test.
-
Entertainment11 hours ago
Mbilia Bel Anusurika Kwenye Ajali ya Barabarani – Kinshasa
-
Entertainment23 hours ago
#COCODRIVE: Crack Sound Siyo Mashine, Ni Vichwa – J Crack Asema Baada ya Kuibiwa Vyombo Studioni Kwake
-
International News20 hours ago
Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni