News
Rais Ruto atia saini mswada wa fedha wa 2025 kuwa sheria.

Rais William Ruto ameidhinisha Mswada wa Fedha wa 2025.
Ruto alitia saini mswada huo kuwa sheria asubuhi ya alhamisi tarehe 26 juni 2025 katika ikulu ya Nairobi baada ya wabunge kupitisha sheria iliyopendekezwa wiki jana.
Ingawa mswada huo uliepuka kuwasilisha ushuru mpya kufuatia maandamano mabaya ya mwaka jana dhidi ya mswada wa fedha wa 2024/2025, baadhi ya vifungu vilikuwa na utata kama vile pendekezo la kutaka kuipa Mamlaka ya kitaifa ya ukusanyaji ushuru KRA uwezo wa kufikia data ya kibinafsi na ya kifedha ya walipa kodi.
Wabunge hatimaye waliuangusha walipokuwa wakiupigia kura kabla ya kutumwa kwa rais Ruto ili kuidhinishwa.
Waziri wa hazina ya kitaifa John Mbadi aliwasilisha bajeti ya shilinghi trilioni 4.2 katika mwaka wa kifedha wa 2025/26 bungeni mapema mwezi huu, na wizara yake inatarajia kukusanya hadi shilingi bilioni 30 katika mapato ya ziada kutoka kwa mswada wa huo wa fedha.
Wakati huo huo, rais Ruto pia alitia saini mswada wa uidhinishaji wa mwaka 2025, utakaoruhusu hazina ya kitaifa kuchukua shilingi trilioni 1.88 kutoka kwa hazina ya pamoja kwa mwaka wa kifedha wa 2025/26.
Mswada huo unaruhusu wizara, idara na mashirika kutumia shilingi bilioni 672 katika ugavi wa msaada, kama ilivyoidhinishwa na bunge.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.
Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.
Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.
Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Mradi wa Galana Kulalu kukabili uhaba wa chakula nchini

Serikali imesema inalenga kufikia ekari 3,200 za kilimo katika mradi wa uzalishaji chakula wa Galana Kulalu ifikapo mwishoni mwa mwaka huu wa 2025.
Waziri wa maji, usafi na kilimo nyunyizi Eric Mugaa alisema tayari ekari 1,060 zimepandwa mahindi kwa kutumia mifumo ya umwagiliaji ya kisasa, mazao ya kwanza yakitarajiwa kuvunwa mwezi Oktoba, huku maandalizi yakuongeza mashamba zaidi yakiendelea.
Akizungumza alipozuru mradi wa Galana Kulalu kutathmini maendeleo ya shughuli za mradi huo, waziri Mugaa pia alisema miundombinu mipya ikiwemo mabwawa ya kuhifadhi maji, mifareji ya kunyunyiza maji, na mitambo ya kusukuma maji imejengwa ilikuwezesha shughuli za unyunyizaji.
Wakati huo huo, waziri huyo alidokeza kuwa ujenzi wa Daraja la Sabaki umefikia hatua ya asilimia 50, akidokezakwamba daraja hilo linatarajiwakukamilika hivi karibuni ili kurahisisha usafirishaji wa vifaa vya kilimo na vile vilekusafirisha mazao kutoka Galana Kulalu.
Serikali kupitia Mamlaka ya unyunyizi iliahidi kuendelea kushirikiana na sekta za kibinafsi kuhakikisha mradi huo wa Galana Kulalu unakuwa suluhu ya uhaba wa chakula hapa nchini.
Taarifa ya Mwanahabari wetu