Connect with us

News

Rais Ruto atia saini mswada wa fedha wa 2025 kuwa sheria.

Published

on

Rais William Ruto ameidhinisha Mswada wa Fedha wa 2025.

Ruto alitia saini mswada huo kuwa sheria asubuhi ya alhamisi tarehe 26 juni 2025 katika ikulu ya Nairobi baada ya wabunge kupitisha sheria iliyopendekezwa wiki jana.

Ingawa mswada huo uliepuka kuwasilisha ushuru mpya kufuatia maandamano mabaya ya mwaka jana dhidi ya mswada wa fedha wa 2024/2025, baadhi ya vifungu vilikuwa na utata kama vile pendekezo la kutaka kuipa Mamlaka ya kitaifa ya ukusanyaji ushuru KRA uwezo wa kufikia data ya kibinafsi na ya kifedha ya walipa kodi.

Wabunge hatimaye waliuangusha walipokuwa wakiupigia kura kabla ya kutumwa kwa rais Ruto ili kuidhinishwa.

Waziri wa hazina ya kitaifa John Mbadi aliwasilisha bajeti ya shilinghi trilioni 4.2 katika mwaka wa kifedha wa 2025/26 bungeni mapema mwezi huu, na wizara yake inatarajia kukusanya hadi shilingi bilioni 30 katika mapato ya ziada kutoka kwa mswada wa huo wa fedha.

Wakati huo huo, rais Ruto pia alitia saini mswada wa uidhinishaji wa mwaka 2025, utakaoruhusu hazina ya kitaifa kuchukua shilingi trilioni 1.88 kutoka kwa hazina ya pamoja kwa mwaka wa kifedha wa 2025/26.

Mswada huo unaruhusu wizara, idara na mashirika kutumia shilingi bilioni 672 katika ugavi wa msaada, kama ilivyoidhinishwa na bunge.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Published

on

By

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.

Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.

Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.

“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

News

Mahakama ya Kilifi yaanzisha upya kesi ya ulaghai wa pesa

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imeanzisha upya kesi ya mwanaume mmoja anayekabiliwa na shtaka la ulaghai wa pesa.

Hii ni baada ya Mwanaume huyo kwa jina Samuel Ngonyo, kuachiliwa kwa dhamana hapo awali lakini alikosa kudhuhuria vikao Mahakamani hali iliyopelekea kesi hiyo kuanzishwa upya.

Hakimu mkuu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa aliagiza jamaa huyo kuzuliwa rumande baada ya agizo la kukamatwa kwake kuidhinishwa na Mahakama baada ya jamaa huyo kupuuza vikao vya Mahakama vya awali.

Kabla ya agizo hilo, Mahakama ilielezwa kwamba mnamo tarehe tofauti kati ya mwezi Septemba hadi Oktoba mwaka 2021 katika maeneo la Ganze kaunti ya Kilifi kwa kutumia njia ya ulaghai, mshukiwa alichukua pesa taslimu shilingi elfu 50 ya mlalamishi Grace Sidi Katana.

Mahakama ilielezwa zaidi kwamba mshukiwa alitekeleza kitendo hicho baada kumdanganya Mlalamishi kwamba yeye ni Mwandishi na afisa wa kazi za umma hivyo angemsaidia Moses Katana mtoto wa mlalamishi kupata kazi ya serikali.

Kesi hiyo itaendelea mnamo tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending